ĐÓMAP”Œșœ

Papa Leo XIV kwa waendesha Baiskeli:mnakaribishwa daima na Kanisa linalowakilisha upendo wa Mungu kwa watu wote!

Papa Leone XIV aliwakaribisha waendesha baiskeli mjini Vatican na kuwambia kuwa wajue wao ni mifano wa kuigwa kwa vijana duniani kote.Giro d'Italia inapendwa kweli na sio Italia tu.Kuendesha baiskeli ni muhimu sana kama ilivyo michezo kwa ujumla.Baadaye walipitia kwenye Bustani,Groto ya Maria wa Lourdes na Monasteri ya Mater Ecclesiae.

Na Angella Rwezaula – Vatican.

Kama ilivyokuwa imepangwa kuhusiana na (Giro d’Italia)mzunguko wa waendesha Basikeli nchini Italia, mpango uliokuwa umekubaliwa hapo awali na Hayati Papa Francisko, Dominika tarehe 1 Juni 2025, saa alasiri, Papa Leo XIV aliwakaribisha ndani ya mji wa Vatican kikundi hicho, kabla ya kuzungukia maeneo ya bustani mjini Vatican. Kwa njia hiyo alitoa maneno mafupi kwao ambapo mwishoni aliwabariki kwa lugha ya kiingereza.

Wawakilishi wa waendesha Baiskeli
Wawakilishi wa waendesha Baiskeli   (@Vatican Media)


Baba Mtakatifu Leo XIV alisema: Habari za asubuhi kwenu nyote! Karibu Vatican! Ni furaha kuwasalimu kwenye hatua hii ya mwisho ya “Giro d'Italia,” yaani “mzunguko wa Italia.” Ninatumaini kuwa ni siku nzuri sana kwenu nyote. Mjue kwamba nyinyi ni mifano ya kuigwa kwa vijana duniani kote. “Giro d'Italia” inapendwa kweli na sio Italia tu. Kuendesha baiskeli ni muhimu sana, kama ilivyo michezo kwa ujumla. Niwakushukuru kwa kila kitu mnachofanya, na ninyi ni mifano ya kuigwa kweli! Na ninatumaini kwamba, kwa kuwa mmejifunza kutunza mwili wenu, roho yenu itabarikiwa kila wakati na kwamba kila wakati mtakuwa makini kwa wanadamu wote: mwili, akili, moyo na roho. Mungu awabariki!”

Papa akipewa Jezi
Papa akipewa Jezi   (@Vatican Media)
Papa akiwasalimia waendesha Baiskeli
Papa akiwasalimia waendesha Baiskeli   (@VATICAN MEDIA)

Mnakaribishwa hapa Vatican

Baba Mtakatifu Leo hakuishia hapo bali hata kwa lugha ya Kiingezea aliwambia kwamba: “Mungu awabariki ninyi nyote katika sehemu hii ya mwisho ya ‘Giro d’Italia.’ Hongereni nyote na mjue kwamba mnakaribishwa daima hapa Vatican, mnakaribishwa daima na Kanisa linalowakilisha upendo wa Mungu kwa watu wote. Na baraka ya Mwenyezi Mungu, Baba, Mwana na Roho Mtakatifu iwafikie ninyi nyote na kukaa nanyi milele. “Waliitika ‘Amina’ kwa Baraka hiyo na kuwapongeza wote: “Hongereni.”

Wakati muhimu wa kuzungukia bustani za Vatican
Wakati muhimu wa kuzungukia bustani za Vatican   (@Vatican Media)
Njia ndani ya Vatican
Njia ndani ya Vatican   (@Vatican Media)

Waendesha Baiskeli ya Mzunguko wa Italia,  baada ya baraka walipata fursa ya kuzungukia Bustani nzuri, kufika hadi, Groto ya Maria wa Lourdes na Monasteri ya Mater Ecclesiae na kurudi nyuma kuendelea na njia yao ya mzunguko uliopangwa.

Wakati wa kutoa ndani ya Vatican
Wakati wa kutoa ndani ya Vatican   (@Vatican Media)
Papa Leo XIV kwa waendesha Baiskeli
01 Juni 2025, 19:10