ミモMAPオシコス

2025.05.06 12テつェ Mkutano wa Makardinali. 2025.05.06 12テつェ Mkutano wa Makardinali.  (@VATICAN MEDIA)

Wito wa makardinali:kujenga amani ya haki na ya kudumu bila kusita!

Tamko la makao makuu ya Vatican wakati wa Mkutano Mkuu kabla ya Uchaguzi wa Papa Mpya: Makardinali wanaonesha wasiwasi wao mkubwa kwa watu ambao bado ni wahanga wa migogoro. Kwa kuzingatia mashambulizi ambayo yameongezeka hasa dhidi ya raia,ombi ni kwa pande zote zinazohusika kufikia usitishaji wa kudumu wa mapigano haraka iwezekanavyo.Mazungumzo bila masharti yametolewa kwa kauli moja.

Vatican News

Katika mkesha wa kuanza kwa Mkutano Mkuu wa uchaguzi, tarehe 6 Mei 2025, Makardinali waliokusanyika mjini Vatican kwa ajili ya kumchagua Papa mpya, walihimiza kusitishwa kwa mapigano katika maeneo ambayo migogoro inaendelea. Wakiwa wamekusanyika katika Mkutano Mkuu, Makardinali, walibainisha kwa masikitiko kwamba 窶徂akuna maendeleo yoyote ambayo yanapatikana katika kukuza michakato ya amani nchini Ukraine, Mashariki ya Kati na sehemu nyingi za dunia窶 na kwa hiyo, wanaelezea 窶忤asiwasi wao kwa mashambulizi ambayo yamezidi hasa dhidi ya raia."

Dunia inatamani amani

Makardinali hao walisisitiza kuwa: "Tunatoa wito wa dhati kwa pande zote zinazohusika kufikia usitishaji wa kudumu wa mapigano haraka iwezekanavyo na kujadiliana, bila masharti na ucheleweshaji zaidi, amani inayotamaniwa kwa muda mrefu na watu wanaohusika na ulimwengu mzima. Mwaliko kutoka kwa Makadinali unaelekezwa kwa waamini wote kuzidisha dua kwa Mola kwa ajili ya amani ya haki na ya kudumu" Ndivyo tunasoma taarifa iliyotolewa na Makao Makuu ya ya mjini Vatican.

Wito wa Makardinali
07 Mei 2025, 15:15