ĐÓMAPµĽş˝

2025.05.22 Sr Tiziana Merletti. 2025.05.22 Sr Tiziana Merletti. 

Papa Leo XIV amemteua Katibu Mkuu wa Baraza la Kipapa la Maisha ya kitawa na kazi za kitume!

Sr.Tiziana Merletti,ambaye aliwahi kuwa Mkuu wa Shirika la Wafransiskani wa Maskini ndiye Katibu Mkuu mpya wa Baraza la Kipapa la Mashirika ya Kitawa na Kazi za kitume.

Vatican News

Baba Mtakatifu Leo XIV, alhamisi tarehe 22 Mei 2025 amemteua Katibu Mkuu wa Baraza la Kipapa la Maisha ya Kitawa na Vyama vya Kitume, Mweshimiwa  Sr Tiziana Merletti,ambaye aliwahi kuwa Mkuu wa Shirika  la Wafransiskani Maskini.

Wasifu wake

Sr. Merletti alizaliwa tarehe 30 Septemba 1959 huko Pineto (TE), Italia. Kunako 1986 alifunga nadhiri za kwanza katika Taasisi hiyo ya Wafransiskani Masikini.

Mnamo mwaka 1984 alipata digrii ya sheria katika Chuo Kikuu Huria cha Abruzo cha (“Gabriele d’Annunzio” huko  Teramo,   na kunako  1992, alipata Udkatari wa Sheria katika Chuo Kikuu cha Kipapa cha Laterano, Roma. Tangu 2004 hadi 2013 alikuwa Mkuu wa Shirika lake la kitawa. Hadi uchaguzi wake ni  Profesa katika Kitengo cha Sheria za Kanoni za Kanisa katika Chuo Kikuu cha Kipapa cha Antonianum,  Roma na kushirikiana katika masuala ya kisheria na Umoja wa Mama wakuu wa Mashirika kimataifa.

Papa amemteua Sr Tiziana Merletti

 

22 Mei 2025, 16:11