ÐÓMAPµ¼º½

Kardinali Reina, Makamu wa Baba Mtakatifu Jimbo kuu la Roma. Kardinali Reina, Makamu wa Baba Mtakatifu Jimbo kuu la Roma.  (VATICAN MEDIA Divisione Foto)

Papa Leo XIV amefanya teuzi mpya

Papa Leo XIV,Mei 19 amefanya teuzi:amemteua Kansela wa Taasisi ya Kipapa ya Taalimungu "Yohane Paulo II" ya Ndoa na Familia na Kansela wa Chuo Kikuu cha Kipapa,Kardinali Reina,Makamu wa Papa Jimbo la Roma.Amemteua Kardinali Bustillo,OFMConv kumwakilisha katika tukio la miaka 350 la Moyo Mtakatifu wa Yesu kwa Alacoque.Amemteua Padre Chicoma Bundo Chico,S.I.,kuwa Mkuu wa Ofisi ya Baraza la Kipapa la Maendeleo Fungamani ya Binadamu.

Vatican News


Baba Mtakatifu Leo XIV, Jumatatu tarehe 19 Mei 2025, amefanya teuzi mbali mbali: Amemteu Kansela wa Taaisisi ya Kipapa la Taalimungu, ya (Yohane Paulo II) kwa ajili ya Sayansi ya Ndoa na Familia, Kardinali Baldassare Reina, Makamu wa Baba Mtakatifu kwa ajili ya Jimb la Roma na Kansela wa Chuo cha Kipapa Laterano.


Baba Mtakatifu amemteua Kardinali François-Xavier Bustillo, O.F.M. Conv., Askofu Mkuu wa Ajaccio, kuwa mwakilishi wake maalum katika hitimisho la Maadhimisho ya miaka 350 ya kutokewa kwa Moyo Mtakatifu wa Yesu kwa Mtakatifu Margherita Maria Alacoque, itakayofanyika katika madhabahu ya Paray-le-Monial, tarehe 27 Juni 2025 huko Ufaransa.


Baba Mtakatifu Leo XIV  aidha amemteua Mkuu wa Ofisi ya Baraza la Kipapa la Huduma ya Maendeleo Fungamani ya Binadamu, Mheshimiwa Padre Avelino Chicoma Bundo Chico, S.I., ambaye hadi uteuzi huo alikuwa ni Afisa wa Ofisi hiyo ya Curia Romana.
 

19 Mei 2025, 14:50