ÐÓMAPµ¼º½

Rais Gitanas NausÄ—da wa Lithuania anashiriki katika hija ya matumaini ya watu wa Mungu kutoka Lithuania. amekutana na kuzungumza na viongozi wakuu wa Vatican. Rais Gitanas NausÄ—da wa Lithuania anashiriki katika hija ya matumaini ya watu wa Mungu kutoka Lithuania. amekutana na kuzungumza na viongozi wakuu wa Vatican.  (VATICAN MEDIA Divisione Foto)

Rais Gitanas Nausèda wa Lithuania Atembelea Mjini Vatican

Kardinali Pietro Parolin, Katibu mkuu wa Vatican akiwa ameambatana na Askofu mkuu Paul Richard Gallagher, Katibu mkuu wa Mambo ya Nchi za Nje, Ushirikiano na Mashirika ya Kimataifa, Jumatatu tarehe 3 Machi 2025 amekutana na kuzungumza na Rais Gitanas Nausėda wa Lithuania, ambaye anashiriki katika hija ya matumaini ya watu wa Mungu kutoka Lithuania. Rais Nausèda anashiriki katika hija ya matumaini ya watu wa Mungu kutoka nchini Lithuania.

Na Padre Richard A. Mjigwa, C.PP.S. – Vatican.

Kardinali Pietro Parolin, Katibu mkuu wa Vatican akiwa ameambatana na Askofu mkuu Paul Richard Gallagher, Katibu mkuu wa Mambo ya Nchi za Nje, Ushirikiano na Mashirika ya Kimataifa, Jumatatu tarehe 3 Machi 2025 amekutana na kuzungumza na Rais Gitanas NausÄ—da wa Lithuania, ambaye anashiriki katika hija ya matumaini ya watu wa Mungu kutoka Lithuania.

Ujumbe wa Lithuania umekutana na ujumbe wa Vatican tarehe 3 Machi 2025
Ujumbe wa Lithuania umekutana na ujumbe wa Vatican tarehe 3 Machi 2025   (VATICAN MEDIA Divisione Foto)

Katika mazungumzo yao, viongozi hawa wameridhishwa na uhusiano wa kidiplomasia kati ya nchi hizi mbili sanjari na mchango wa Kanisa katika ustawi, maendeleo na mafao ya watu wa Mungu nchini Lithuania. Baadaye, viongozi hawa wamejielekeza zaidi katika masuala ya kikanda na kimataifa mintarafu mchakato wa kutafuta na kukuza amani nchini Ukraine.

Kard. Parolin

 

04 Machi 2025, 15:43