ÐÓMAPµ¼º½

Kardinali Parolin Katibu wa Vatican. Kardinali Parolin Katibu wa Vatican.  (Daniele Scudieri - Imagoeconomica)

Kard.Parolin: Kutangazwa kuachiliwa kwa wafungwa wa Cuba ni ishara ya matumaini makubwa

Katibu wa Vatican aliyehojiwa na vyombo vya habari vya Vatican juu ya habari kutoka Havana nchini Cuba:“Tunatumaini kuwa 2025 itaendelea katika mwelekeo huu na kwamba habari njema itaongezeka, hasa kwa kusitishwa kwa migogoro mingi ambayo bado inaendelea."

Vatican News

Kardinali Pietro Parolin, Katibu wa Vatican akihojiwa na  vyombo vya habari vya Vatican alipokuwa nchini Ufaransa kuhusiana na taarifa ya Havana alisema kuwa: "Habari za kuachiliwa polepole kwa wafungwa 553 wa Cuba ni ishara ya matumaini makubwa mwanzoni mwa Jubilei hii. Ni muhimu kwamba mamlaka ya Havana wameunganisha uamuzi huu moja kwa moja na wito wa  Papa ambazo zimetokea mara kadhaa wakati wa Mwaka Mtakatifu."

Katibu wa Vatican aidha aliongeza kusema: "Mwaka 2024 ulimalizika kwa Rais wa Marekani kubadilisha makumi ya hukumu za kifo hadi kifungo cha maisha, na kwa habari kwamba Zimbabwe ilikuwa imefuta hukumu ya kifo. Tunatumaini kuwa 2025 itaendelea katika mwelekeo huu na kwamba habari njema itaongezeka, hasa kwa kusitishwa kwa migogoro mingi ambayo bado inaendelea."

Maoni ya Kardinali Parolin kuhusu CUBA
16 Januari 2025, 09:54