ĐÓMAPµĽş˝

2024.08.24:Kardinali Parolin alimweka wakfu wa kiaskofu Mons.Kryspin Dubiel, Balozi Mpya wa Vatican wa Angola na SĂŁo TomĂ© na PrĂ­ncipe. 2024.08.24:Kardinali Parolin alimweka wakfu wa kiaskofu Mons.Kryspin Dubiel, Balozi Mpya wa Vatican wa Angola na SĂŁo TomĂ© na PrĂ­ncipe.  (Radio Fara tv)

Kard.Parolin kwa Dubiel:Unaitwa kuungana naye kwa nguvu zaidi!

Kardinali Pietro Parolin,Katibu wa Vatican aliongoza ibada ya misa Takatifu ya kumweka wakfu wa kiaskofu wa Kryspin Dubiel kuwa Askofu tarehe 24 Agosti huko Leżajsku,Poland.Huyo ni Padre wa Jimbo la Przemyśl,aliyeteuliwa na Baba Mtakatifu kuwa Balozi wa Angola na São Tomé na Príncipe hivi karibuni.

Na Angella Rwezaula – Vatican.

“Shika amana ya imani ya kitume uliyokabidhiwa, ilinde kama msimamizi mwema na ueneze hazina yake kwa upana, ili, kama mbegu njema, izae matunda katika Kanisa na katika mashirika ya kiraia. Ni maneno ya  Kardinali Parolin, Katibu wa Vatican yaliyosikika  wakati wa mahubiri yake kwenye misa ya kuwekwa wakfu wa kiaskofu wa Mons. Kryspin Dubie, tarehe 24 Agosti 2024 huko LeĹĽajsku nchini Poland.Huyo ni Padre wa Jimbo la PrzemyĹ›l, aliteuliwa na Baba Mtakatifu kuwa Balozi wa Angola na São Tomé na Príncipe hivi karibuni.

Kardinali Parolin wakati wa mahubiri 24 Agosti 2024
Kardinali Parolin wakati wa mahubiri 24 Agosti 2024   (Radio Fara tv)

Katika mahubiri, Kardinali Parolin alikumbuka jinsi ilivyo “muhimu kwa watu wa nyakati hizi zilizochanganyikiwa kutangaza kwamba Bwana amechukua asili ya mwanadamu na ameikomboa bila shaka, amechukua umiliki wa ukweli wetu mara moja na kwa wote. Kwa hiyo, jitihada zetu za kujenga jiji la kiulimwengu hazifai kitu ikiwa tutatenga uwepo wa Mungu kutoka humo.”

Misa ya kuwekwa wakfu wa kiaskofu wa Mons Dubiel
Misa ya kuwekwa wakfu wa kiaskofu wa Mons Dubiel   (Radio Fara tv)

Akizungumzia kuhusu Askofu mkuu mpya huyo na Balozi wa Kitume na kukumbuka “njia yake ya ufundi na huduma ya ukuhani”, alikumbuka kwamba “alikuwa amepitia hamu ya kuimarisha ujuzi wake na kubaki mwaminifu kwa Bwana. Sasa Bwana, ambaye anajua maisha yake ya nyuma, anamwita kuungana naye kwa nguvu zaidi.” Kardinali Parolin pia alizungumza kuhusu wajibu wa Balozi mpya wa Kitume kwamba “Ni huduma inayotolewa kwa manufaa ya Kanisa na kwa ajili ya amani duniani. Huduma na ubalozi wake utazaa matunda zaidi kadiri anavyoungwa mkono kwa uthabiti na sala na tafakari ya Neno la Mungu.”

Wakati wa Litania kwa ajili ya kuwekwa wakfu wa kiaskofu kwa Mons.Dubiel
Wakati wa Litania kwa ajili ya kuwekwa wakfu wa kiaskofu kwa Mons.Dubiel   (Radio Fara tv)

Maadhimisho hayo yalifanyika katika Basilika Ndogo huko LeĹĽajsk nchini Poland ambapo Askofu Mkuu Dubiel anazaliwa. Kwa njia hiyo Maaskofu na Makardinali StanisĹ‚aw Dziwisz na Kazimierz Nycz pia walishiriki katika liturujia, pamoja na Askofu Mkuu Antonio Filipazzi, balozi wa Vatican nchini Poland, vile vile Askofu Marek Marczak, katibu mkuu wa Baraza la Maaskofu wa Poland. Wakonselebranti walikuwa Askofu Mkuu  Salvatore Pennacchio, rais wa Chuo cha Kipapa cha Kikanisa na Askofu Mkuu  Adam Szal, wa Jimbo Kuu la PrzemyĹ›l nchini Poland.

Kardinali Parolin akibariki waamini
Kardinali Parolin akibariki waamini   (Radio Fara tv)
Kardinali Parolin alimweka Wakfu wa kiaskofu Mons.Dubiel

 

26 Agosti 2024, 14:57