MAP

2023.08.02 Papapa amefika Ureno hii ni gwaride ya heshima. 2023.08.02 Papapa amefika Ureno hii ni gwaride ya heshima.  (ANSA)

WYD Lisbon 2023:Papa Francisko amefika Ureno

Baba Mtakatifu Francisko amefika nchini Ureno katika fursa ya siku ya XXXVII ya Vijana duniani na kwa hiyo kama ziara yake ya 42 ya kitume kimataifa.Akiwa njiani ametuma telegram kwa marais wa Italia, Ufaransa na Hispania.Amewasalimu waandishi wa habari 80 wanaombatana naye.

Na Angella Rwezaula, - Vatican.

Takriban dakika kumi na tano mapema kuliko muda uliopangwa, Baba Mtakatifu Francisko aliwasili saa 3.43 kwa saa za huko na saa (4.43 nchini Italia), ambapo alitua katika uwanja wa ndege wa Figo Maduro huko Lisbon, katika ziara yake ya kimataifa ya 42 na ikiwa ni kwa mara ya pili nchini Ureno  Mara ya kwanza ilikuwa ni mnamo Mei 2017 wakati wa maadhimisho ya  miaka 100 tangu kutokea kwa Mama Yetu wa Fatima 1917 na hivyo sasa  Baba Mtakatifu atashiriki Siku ya 37 ya Vijana Duniani na vijana milioni wanaotarajiwa humo.

Papa Francisko akiwa anatia saini kitabu cha wageni kwa Rais
Papa Francisko akiwa anatia saini kitabu cha wageni kwa Rais   (VATICAN MEDIA Divisione Foto)

Msemaji wa Vyombo vya habari Vatican Dk. Matteo Bruni ametoa taarifa kuhusu Mkutano wa Papa Francisko katika nyumba ya Mtakatifu Marta kabla ya kuondoka kwenda Lisbon, tarehe 2 Agosti 2023. Katika taarifa hiyo Dk. Bruni mesema kuwa: “leo asubuhi katika Nyumba ya Mtakatifu Marta, kabla ya kuondoka kwenda Lisbon, Papa Francisko amewasalimia watu kama 15 na miongoni mwake, kulikuwa na baadhi ya vijana, wasichana na wavulana ambao wako wanaishi kipindi maalum katika Jumuiya ya kujijua na hivyo hawana uwezo wa kushiriki Siku ya vijana. Hawa waliambatana na babu na bibi  watatu na wajuu wao. Mkutano huo ni  sehemu ya Siku ya Kimataifa ya Bibi na Babu na wazee iliyoadhimishwa hivi karibuni kwa kutaka kusisitiza uhusiano kati ya vizazi, ambapo wanaweza kusaidiana pamoja na kujifunza kutoka mmoja na mwingine”.

Ziara ya Papa nchini Ureno katika WYD

Telegram za Papa

Baba Mtakatifu Francisko akiwa katika ndege, kuelekea Ureno kama kawaida yake, ametuma telegram kwa viongozi wakuu wa nchi ambazo ndege inapitia. Kwanza kabisa kwa Rais wa Jamhuri ya Italia Segio Mattarella kwamba:“ katika wakati ambapo ninajiandaa kuondoka kwenda  Ureno katika fursa ya Siku ya vijana duniani; kwa kuhuishwa na furaha ya kukutana na vijana kutoka kila upande wa dunia kwa kuongozwa na imani na shuku ili kuinuka na kujiweka katika mwendo kuwa na  nguvu za kukutana na Kristo na ili waweza kutiwa moyo katika kutafuta ukweli na maana ya maisha". Kwa hakika katka kushirikishana tumaini hili na wewe Bwana Rais, nimependelea kukutumia salamu zangu za dhati ambazo zisambazwe kwa waitalia wote kwa kukusindizwa kwa sala na matashi mema na matarajio!

Na telegram kwa Rais wa Ufaransa, Baba Mtakatifu  Francisko ameandika kuwa: “ Nimepitia juu ya Ufaransa kwa ndege nikiwa njiani kueleka Ureno, ninakutumia salamu za matashi mema mhesh. na wazalendo wote kwa pamoja nikiwahakikisha sala zangu na kwa amani na ustawi wa taifa.” Kwa upande wa Rais wa Hispania, Baba Mtakatifu Francisko ameandikia Mfalme Pilipe VI kuwa: “Ninakutumia  salamu zangu  na wajumbe wote wa familia ya kifalme na watu wa Hispania, nikiwa juu ya nchi yako kuelekea Ureno. Ninakuhakikishia wewe uhakika wa sala zangu na juu ya yako ninakupa baraka kutoka kwa Mungu kwa ajili ya utulivu na furaha.

Ujumbe wa Rais Mattarella wa Italia

Rais wa Jamhuri ya Italia, Bwana Sergio Mattarella,naye  amemtumia Baba Mtakatifu Francisko kama jibu la ujumbe wake: “Ninataka zikufikie kwa dhati shukrani kwa ajili ya ujumbe ulionitumia katika wakati huu ambao unajiandaa kwenda Ureno”. Ziara ya kitume katika fursa ya Siku ya XXXVII  ya Vijana duniani, inawakilisha fursa maalum ya kukutana na vijana wengi kutoka kila pande ya ulimwengu ambayo itashuhudia urafiki na katika imani ya kuamini wakati ujao na utashi wa vijana katika  ulimwengu jumuishi zaidi na mshikamano. Ninakuelekeza Baba Mtakatifu wazo langu la kina kwa kuungana na mwelekeo wa kina kwako”.

Ziara ya 42 ya kitume

Kwa  hiyo imeanza ziara ya 42 ya kitume ya Papa Francisko. Nchi ya Ureno iliyokuwa ikimsubiri Mfuasi wa Petro imekuwa na furaha kubwa kukaribisha Siku ya vijana duniani ambayo ilifunguliwa kwa ibada ya misa takatifu tarehe Mosi Agosti 2023 jioni jijini Lisbon.  Misa ihiyo iliongozwa na Patriaki wa mji wa Lisbon,  Kardinali Manuel Clementj. Kwa mujibu wa takwimu za ndani kuhusiana na washiriki itakuwa ni milioni moja ya vijana, ambapo pamoja na siku hiyo Baba Mtakatifu anatarajiwa kwenda huko Fatima katika madhabahu ya Mama Yetu wa Fatima ili kusali kwa ajili ya Amani akiwa na mahujaji wagonjwa  mnamo  Jumamosi tarehe 5 Agosti 2023.

Salamu wakati akiwa kwenye ndege

Baba Mtakatifu akiwa katika ndege kama kawaida yake amewasalimu na kuzungumza na waandishi wa habari wanaombatana naye katika hija hii.  Aidha kulikuwa na barua moja ambayo Eva Fernández wa Radio Cope amemkabidhi Papa iliyoandikwa na kijana Pablo, wa Hispania mwenye wa miaka  21 aliyetamani sana kushiriki Siku ya vijana duniani  lakini kwa bahati mbaya tarehe 15 Julai 2023 aliaga dunia kutokana na saratani, baada ya kuwa amejiunga na shirika la wakarmeli. Katika maneno yake ni yana matumaini kwa ajili ya vijana wote wanaoshiriki tukio hilo Lisbon na shauku ya kijana aliyempenda Yesu kwa dhati.

Dk Bruni na Papa wakati wa salamu kwa waandishi wa habari kwenye ndege
Dk Bruni na Papa wakati wa salamu kwa waandishi wa habari kwenye ndege   (VATICAN MEDIA Divisione Foto)

Kwa hiyo Papa Francisko amewasalimia karibu waandishi 80 wanaomsindikiza katika ziara hii ambapo Dk Bruni wakati anatoa utangulizi alisema kuwa karibu ndege imejaa na kwamba kwa uhakika kuna umati mkubwa Ureno ambao unasubiri kwa upande wa waandishi, kwa ishara na maneno yake kwa siku hizi. Na kwa upande wa Papa Francisko amesema: “Habari za asubuhi na asante  kwa sindikizo hili na kwa ajili ya kazi zenu na sasa ninasalimia mmoja baada ya mwingine, asante,” alihitimisha.

02 Agosti 2023, 12:29