ÐÓMAPµ¼º½

Papa leo XIV Papa leo XIV  (@Vatican Media)

Papa kuhusu shambulio la Israel dhidi ya Hamas nchini Qatar:"Hali ni mbaya sana"

Akiondoka kwenye makazi yake huko Castel Gandolfo,alikokwenda jana usiku,Papa Leo XIV alijibu kwa ufupi maswali ya waandishi wa habari kuhusu shambulio la bomu huko Doha:"Hatujui mambo yanaenda wapi.Ni lazima tuombe sana na kuendelea kufanya kazi na kusisitiza amani."Kuhusu agizo la kuhama katika Jiji la Gaza,Papa alisema alijaribu kuwasiliana na paroko:"Sina habari."

Vatican News

Papa Leo XIV alizungumzia "habari nzito kweli," akimaanisha mashambulizi ya Israel dhidi ya viongozi kadhaa wa Hamas huko Doha, Qatar. Shambulio hilo lilipiga majengo kadhaa ya makazi katika mji mkuu. Papa alihojiwa na vyombo vya habari  Jumanne tarehe 9 Septemba 2025,  nje ya Eneo la Villa Barberini, makazi yake huko Castel Gandolfo, ambapo aliamua kutumia chini ya siku moja, kuanzia jana jioni tarehe 8 Septemba hadi mchana wa Jumanne Septemba 9, 2025.

Kuomba kwa Bidii na Kufanya Kazi kwa ajili ya Amani

Alisimama kwa muda mfupi na waandishi wa habari mbele ya lango kuu, huku msururu mrefu wa watu ukimpigia makofi na kuimba jina lake, ambapo Papa Leo XIV, akijibu maswali kwenye waandishi wa Runinga ya Italia ( Rai News,) alionesha wasiwasi wake kwa kile kinachotokea Mashariki ya Kati: "Hali nzima ni mbaya sana," alisema. "Hatujui mambo yanakwenda wapi; siku zote ni mbaya. Ni lazima tuombe kwa bidii na kuendelea kufanya kazi, kutafuta na kusisitiza amani."

Agizo la Uokoaji huko Gaza

Kuhusu agizo la Israel la kuhama mara moja kwa wakazi wa Mji wa Gaza kwa kutarajia kuongezeka kwa operesheni za kijeshi, Papa alieleza kuwa alijaribu kuwasiliana na Paroko wa Familia Takatifu, Padre Gabriel Romanelli. "Nilijaribu kumpigia simu Padre wa parokia sasa, lakini sina habari," alisema. "Kwa hakika walikuwa sawa, lakini baada ya utaratibu huu mpya, sina uhakika."

Kurudi Vatican.

Baba Mtakatifu  Leo XIV kisha alisalimiana na baadhi ya waamini waliokuwepo kabla ya kurejea Mjini Vatican. Alifika Castel Gandolfo jana jioni  tarehe 8 Septemba na alitumia asubuhi na alasiri huko, na kutekeleza majukumu yake ya siku ambayo hakuna vikao vilivyopangwa.

Papa ajibu maswali ya waandishi wa habari
09 Septemba 2025, 18:08