ÐÓMAPµ¼º½

Roho ya Marehemu Pascale Rafic,kijana wa Misri ipumzike kwa Amani,Amina. Roho ya Marehemu Pascale Rafic,kijana wa Misri ipumzike kwa Amani,Amina. 

Papa anatoa salamu za rambirambi kwa kijana wa Kimisri aliyefari safari kuja Roma

Papa Leo XIV atoa salamu na masikitiko yake ya kiroho kwa familia ya Pascale Rafic,aliyeaga dunia akiwa safarini na kundi lake ili kushiriki Jubilei ya Vijana.Jumamosi asubuhi,Agosti 2,Papa alikutana mjini Vatican na vijana wenzake katika kundi hilo,ili kutoa rambirambi na faraja kwa Jumuiya nzima alikokuwa anatoka Nchini Misri.

Vatican News


Baba Mtakatifu Leo XIV, Jumamosi tarehe 2 Agosti 2025 amehuzunisha na habari za kifo cha ghafla cha kijana mmoja wa miaka 18 aitwaye Pascale Rafic, kilichotokea akiwa safarini kuja Roma akitokea Misri ili kuweza kushiriki Jubilei ya vijana.

Wawakilishi wa kundi la vijana kutoka Misri waliompoteza kijana mwenzao
Wawakilishi wa kundi la vijana kutoka Misri waliompoteza kijana mwenzao   (@Vatican Media)

Papa Leo XIV aliwasiliana na Askofu Jean-Marie Chami, wa Jimbo la Tarso na msaidizi wa Kanisa la Upatriaki wa Antiokia ya Kigiriki-Melkiti kwa ajili ya Misri, Sudan na Sudan Kusini, kuelezea ukaribu wake wa kiroho na kwa familia ya kijana huyo ikiwa ni pamoja na jumuiya nzima.

Sala ya kumwombea kijana wa Misri aliyefariki dunia akiwa safarini kuja Roma
Sala ya kumwombea kijana wa Misri aliyefariki dunia akiwa safarini kuja Roma   (@Vatican Media)

Baba Mtakatifu Leo XIV vile vile katika siku ya Jumamosi, tarehe 2 Agosti, asubuhi, alikutana na kikundi cha wanahija, waliokuwa safarini na kijana huyo aliyefariki dunia. Mkutano huo uliashirika hisia kali na ulikuwa na fursa ya kusali kwa ajili ya Roho ya marehemu na kukabiliana kiroho kwa ajili ya kijana huyo ambapo bado wameshtushwa kwa uchungu na tukio hilo.

Kundi la vijana liliompoteza kijana mwenzao wakati wa kuja Roma
Kundi la vijana liliompoteza kijana mwenzao wakati wa kuja Roma   (@Vatican Media)

Kwa ushiriki uchungu huo, na wale wote ambao wamekumbwa na mkasa huo wa ajabu, Baba Mtakatifu Leo XIV aliwakikishia sala zake na kuomba Bwana nguvu na faraja kwa ajili ya familia, marafiki na wote ambao wanaomboleza kwa kumpoteza kijana huyo.

Kukutana na vijana wa Misri na Papa
Kukutana na vijana wa Misri na Papa   (@Vatican Media)
Papa na rambi rambi kwa ajili ya kijana wa Misri.


 

02 Agosti 2025, 12:48