MAP

Papa Leo XIV awatembelea Jumuiya ya Mtakatifu Agostino kwa siku ya kuzaliwa kwa Mkuu wa Shirika!

Baada ya Ibada ya Misa Takatifu ya Jubilei ya Familia,Watoto,babu,bibi na Wazee,Papa Leo XIV,Dominika Juni 1 alifika katika Chuo cha Kimataifa cha Mtakatifu Monica kilicho mita chache na Vatican na akasimama kwa chakula cha mchana katika kuadhimisha miaka 70 ya kuzaliwa kwa Padre Alejandro Moral, rafiki yake wa siku nyingi na Mkuu wa shirika la Mtakatifu Agostino.

Vatican News

Baada ya Ibada ya Misa Takatifu katika Uwanja wa Mtakatifu Petro kwa ajili ya Jubilei ya familia, watoto, babu, bibi na wazee, Baba Mtakatifu Leo XIV, Dominika tarehe 1 Juni 2025 aliwafikia jumuiya ya kitawa, kupitia njia ya Paolo VI; ambapo wanafunzi wa Shirika la Mtakatifu Agustino kutoka nchi mbalimbali duniani na baadhi ya walimu wa Taasisi ya Kipapa la Baba wa Kanisa wanaishi, kushiriki katika hafla iliyoandaliwa kuadhimisha miaka 70 ya kuzaliwa kwa Mkuu wa Shirika la Mtakatifu Agostino Padre Alejandro Moral.

Padre Alejandro Moral akimkaribisha Papa mara baada ya kufika
Padre Alejandro Moral akimkaribisha Papa mara baada ya kufika   (©Osafund - Fondazione Agostiniani nel Mondo)

Njia Sambamba

Urafiki wa muda mrefu unawafunga Papa na Padre Alejandro, mzaliwa wa La Vid, Hispania, tarehe 1 Juni 1955. Wawili hao walikutana miaka ya 1980 jijini Roma, katika Chuo cha Mtakatifu Monica, walipokuwa wakisoma Sheria kwa  Provost, katika Chuo Kikuu cha Kipapa cha Mtakatifu Thomas wa Aquinas na Taasisi ya Maandiko Matakatifu ya Maadili katika Chuo Kikuu cha Kipapa Gregoriana. Njia zao zilitengana mwaka 1985, pale ambapo Padre kijana Robert, aliyepewa daraja la Upadre mwaka 1982, alipotumwa kwenye utume wa Kiagostiniani, Chulucanas, huko Piura, Peru, wakati Padre Alejandro alipomaliza masomo yake akarejea Hispania. Watu hao wawili  walikutana tena jiji  Roma mwaka wa 2001, kwa ajili ya Mkutano Mkuu wa Waagostiniani.

Miaka 70 ya Padre Alejandro Moral Mkuu wa Shirika la Waagostiniani Duniani
Miaka 70 ya Padre Alejandro Moral Mkuu wa Shirika la Waagostiniani Duniani   (©Osafund - Fondazione Agostiniani nel Mondo)

Njia tofauti, dhamana iliyobaki

Alipochaguliwa kuwa Mkuu wa Shirika, Padre Prevost alimchagua Moral kama makamu na akimthibitisha pia katika muhula wake wa pili. Kwa miaka 12 walifanya kazi bega kwa bega na urafiki wao ukukua na kuimarika. Uhusiano wa kidugu ambao unadumu hata wakati njia zao zimegawanyika tena. Mnamo mwaka wa 2013, mwishoni mwa muhula wa pili wa miaka sita kuwa Mkuu wa Shirika la Mtakatifu Agostino, Padre Prevost alirudi katika kanda yake ya kiagostino huko Chicago, wakati Padre  Moral akateuliwa kuwa Mkuu wa  97 Shirika shirika hilo.

Wakati muhimu wa kushiriki Chakula katika kuadhimisha miaka 70 ya Mkuu wa shirika la waagostiniani
Wakati muhimu wa kushiriki Chakula katika kuadhimisha miaka 70 ya Mkuu wa shirika la waagostiniani   (Order of Saint Augustine)

Na ikiwa mwaka mmoja baadaye Padre Robert Prevost aliteuliwa na Papa Francisko kuwa msimamizi wa kitume wa jimbo la Chiclayo, nchini Peru, na baadaye kuteuliwa kuwa Askofu na  wakati huo upendo wa kiagostiniani ulibaki kwa Padre Alejandro, urafiki huo uliosifiwa sana na Baba wa Kanisa Agostino aliyependa maisha ya pamoja katika: “umoja wa akili na moyo” (Utawala)“kutafuta pamoja, kwa upatanisho kamili” na Mungu, ili yeyote aliyeipata ukweli kwanza aweze kuwaongoza wengine ....." ( Maandiko ya Mtakatifu Agostino Solil. 1, 12, 20-13, 22.)

Papa atembelea Jumuiya ya waagostino katika siku ya kuzaliwa kwa Mkuu wa Shirika la Waagostiniani
01 Juni 2025, 14:15