ÐÓMAPµ¼º½

2025.05.20 Baraza la Kipapa la Maaskofu. 2025.05.20 Baraza la Kipapa la Maaskofu.  (@Vatican Media)

Papa Leo XIV atembelea Baraza la Kipapa la Maaskofu

Jumanne tarehe 20 Mei 2025,Baba Mtakatifu Leo XIV alikwenda katika Baraza la Kipapa la Maaskofu ambalo ameliongoza kama Mwenyekiti wake kwa zaidi ya miaka miwili.Katika kikanisa aliadhimisha Misa Takatifu.

Vatican News

Jumanne asubuhi tarehe 20 Mei 2025 Baba Mtakatifu Leo XIV alitembelea Baraza  la Kipapa la Maaskofu kwa kushitukiza ambako aliadhimisha Misa katika kikanisa hicho. Haya yalitangazwa na Ofisi ya Vyombo vya Habari vya Vatican.

Katika makao makuu yaliyoko katika Uwanja wa Pio XII ambayo alikuwa Mwenyekiti wake tangu kuteuliwa kwake kunako tarehe 30 Januari 2023 hadi kuchaguliwa kwake kuwa Papa Leo XIV. Alifika karibu saa 4.00 asubuhi marija ya Ulaya ndani ya gari ndogo jeusi ambalo tayari limeonekana kwa ziara zake nje ya Vatican.

Misa katika Baraza la Kipapa la Maaskofu
Misa katika Baraza la Kipapa la Maaskofu   (@Vatican Media)

Ya kwanza mnamo tarehe 10 Mei 2025, huko Genazzano, kusali katika Madhabahu ya Mama wa Shauri Jema, na ile ya Juma moja kabisa iliyopita alipokwenda Nyumba Mama ya Shirika la Waagostiniani ambapo aliadhimisha Misa na kula chakula cha mchana na ndugu zake wa Waagostiniani.

Kwa njia hiyo, safari hii ilikuwa ya tatu ya kushangaza iliyosalimiwa na makofi na nyimbo za "Viva il Papa" kutoka katika umati mdogo uliokusanyika kwenye Uwanja mita chache kutoka kwenye nguzo za Mtakatifu Petro na Watu wengine walikusanyika katika njia ya Corridori, kwa hiyo nyuma ya jengo, kusubiri gari na Papa kuondoka kwenye eneno hilo, baada ya saa moja na nusu.

Misa ya Papa katika Baraza la Kipapa la Maaskofu
Misa ya Papa katika Baraza la Kipapa la Maaskofu   (@Vatican Media)
Papa katika Baraza lake
20 Mei 2025, 15:07