ĐÓMAPµĽş˝

Papa akutana na marais wa Ukraine na Peru

Katika siku ya mwanzo wa huduma ya mfuasi wa Petro,Baba Mtakatifu Leo XIV alikutana na rais wa Jamhuri ya Peru Bi Dina Ercilia Boluarte Zegarra na Raia wa Ukraine Zelensky.

Vatican News

Baba Mtakatifu Leo XIV alikuwa na mikutano miwili mjini  Vatican nje ya  maadhimisho ya Ekaristi  katika mwanzo wa huduma ya Mtakatifu Petro, Dominika tarehe 18 Mei 2025.

Kwanza alimsalimia Rais wa Peru Bi Dina Ercilia Boluarte Zegarra ambaye aliandika kwenye X kwamba amempelekea Papa ukaribu wa upendo wa watu wa Peru. Kisha akamkumbuka Askofu mpya wa Roma, kama “mtumishi wa Mungu aliyejitolea miaka mingi kwa ajili ya utume wa Injili na kuwahudumia wahitaji zaidi nchini.”

Papa Leo XIV na Rais wa Ukraine na mkewe
Papa Leo XIV na Rais wa Ukraine na mkewe   (@Vatican Media)

Baadaye Baba Mtakatifu Leo XIV alikutana na Rais wa Ukraine, Volodymyr Zelensky pamoja na mkewe Olena Zelenska.

Papa akutana na rais wa Ukraine na mkewe
Papa akutana na rais wa Ukraine na mkewe   (@Vatican Media)

Pia rais huyo aliandika kwenye ukurasa wake wa X shukrani zake kwa maneno yaliyotamkwa kwenye sala ya Malkia wa Mbingu  kuhusu Ukraine hasa "kuhusu hitaji la amani ya haki" kwa sababu "kila taifa linastahili kuishi kwa amani na usalama."

Kisha katika ukuras huo alitoa matashi mema ya utume anaoitiwa Papa kwa matumaini kwamba, sala za "amani ya haki na maisha ya utu kwa wote zitasikika.”

Papa na rais wa Peru na Ukraine
18 Mei 2025, 16:47