ÐÓMAPµ¼º½

Ilikuwa tarehe 13 Mei  1981 wakati Mtakatifu Yohane Paulo II aliposhambuliwa na risasi. Ilikuwa tarehe 13 Mei 1981 wakati Mtakatifu Yohane Paulo II aliposhambuliwa na risasi. 

Misa ya kumbukizi ya kupigwa risasi Papa Yohane Paulo II

Liturujia ya Ekaristi,ilifanyika saa 12 jioni,ikiongozwa na Kardinali Stanislaw Dziwisz,ambaye miaka 44 iliyopita alikuwa karibu na Papa Wojtyla alipopigwa risasi.Baada ya Misa,yalifanyika maandamano hadi kaburi la Papa wa Poland.Ilikuwa ni tarehe 13 Mei 1981 wakati Papa Yohane Paulo II alipopigwa risasi katika Uwanja wa Mtakatifu Petro.

Vatican News

Miaka 44 iliyopita, kunako tarehe 13 Mei 1981, Mtakatifu Yohane  Paulo II alikuwa mwathirika wa shambulio katika Uwanja wa Mtakatifu Petro mjini Vatican. Ili kukumbuka  tukio hilo, Jumanne tarehe 13 Mei  2025, saa 12 jioni masaa ya Ulaya katika Kanisa kuu la Mtakatifu Petro mjini Vatican, Kardinali Stanislaw Dziwisz ambaye wakati huo alikuwa katibu wa Papa wa Poland, aliongoza Ibada ya Misa Takatifu kwenye Kiti cha Mtakatifu Petro na kukiwa na ushiriki wa wazi kwa wote. Baada ya adhimisho la kiliturujia, yalifanyika maandamano kutoka kwenye madhabahu ya Mtakatifu Petro hadi kwenye kaburi la Mtakatifu Yohane Paulo wa Pili liliko pembeni kulia mwa Kanisa Kuu hilo.

Siku ya kupigwa risasi kwa Papa Yohane Paulo II
Siku ya kupigwa risasi kwa Papa Yohane Paulo II

Piazza San Pietro nel giorno dell'attentato a Papa Wojytla.

Siku aliyopshabuliwa na risasi Mtakatifu Yohane Paulo II

Risasi ziligeuzwa na mkono wa Mpaji tu

Siku hiyo mnamo mwaka 1981, saa 11:17 jioni., Papa Wojtyla alikuwa akizunguka katika Uwanja akiwa juu ya Gari la Papa (ÐÓMAPµ¼º½mobile )mbele waamini walioudhuria Katekesi ya Jumatano, wakati alipoanguka ghafla, akijeruhiwa na risasi zilizofyatuliwa na Ali Agca. Papa alihamishiwa mara moja haraka katika hospitali ya Gemelli jijini Roma. Alifanyiwa upasuaji, akipambana na  uhai wake, na akaokolewa. Daima alikuwa na imani kwamba ni Mama Yetu wa Fatima, ambaye ukumbusho wake wa kiliturujia huadhimishwa kila ifikapo Mei 13, ambaye "amepindua risasi" na kuokoa maisha yake.

Un bossolo dei proiettili esplosi da Ali Agca.

Vikasha  vya maganda ya risasi zilizorushwa na Ali Agca.

Msaada wa Mama wa Mbinguni


Mwaka mmoja baada ya shambulio hilo, Mtakatifu Yohane  Paulo II alitembelea Madhabahu ya Fatima kumshukuru Bikira. Aliwaambia waamini waliokuwa wakimsikiliza: "Ningependa kuwaambia kwa ujasiri kwamba wakati shambulio lilifanyika mwaka mmoja uliopita katika Uwanja wa Mtakatifu Petro, nilipopata fahamu, mawazo yangu mara moja yalikimbilia kwenye Madhabahu hii kutoa shukrani kwa Moyo wa Mama wa Mbinguni. Katika yote yaliyotokea, niliona - na nitarudia tena na tena - ulinzi maalum wa uzazi wa Maria."

Kumbukizi ya miaka 44 alipopigwa risasi Papa Yohane Paulo II
14 Mei 2025, 13:14