Picha za ufungaji wa bomba la kupitisha moshi juu ya paa la kikanisa cha Sistine
Vatican news
Picha zilizosambazwa na Vyombo vya Habari vya Vatican zinalionesha uwekaji wa chimney na bomba la kupitisha moshi. Ni zoezi lililofanyika asubuhi tarehe 2 Mei 2025. Ni kutokana na bomba hilo la moshi kwamba, katika siku zijazo, ulimwengu utasubiri kuona ishara itakayokuwa inasubiriwa kwa muda mrefu kuona moshi mweupe, kama ishara ya kuchaguliwa kwa mrithi wa Papa Francisko.
Chimney, iliyounganishwa na majiko mawili ndani ya kikanisa, ni mahali ambapo moshi hutatokea: ule mweusi, kuelezea kwamba hado haijafikia idadi ya takwimu za kura zinazopaswa za thuluthi mbili na moshi mweupe kwa kuashirikia ukamilifu wa uchaguzi wa Papa mpya.
Kura nne zimepangwa kufanyika kwa siku, mbili asubuhi na mbili alasiri, na baada ya kura ya 33 au 34, kwa hali yoyote, kutakuwa na moja kwa moja, na duru ya pili ya lazima kati ya makardinali wawili waliopata kura nyingi zaidi katika kura ya mwisho. Hata katika muktadha huu, hata hivyo, wingi wa theluthi mbili utakuwa muhimu kila wakati.
Makardinali wawili waliosalia katika kinyang'anyiro hicho hawataweza kushiriki kikamilifu katika upigaji kura. Iwapo kura za mgombea zitafikia thuluthi mbili ya waliopiga kura, uchaguzi wa Papa utakuwa halali kisheria.