ÐÓMAPµ¼º½

Uwanja wa Makao makuu ya Manispaa ya mjini wa Roma na mbele yake kuna sanamu ya Marco Aurelio. Uwanja wa Makao makuu ya Manispaa ya mjini wa Roma na mbele yake kuna sanamu ya Marco Aurelio.  (Copyright © Nicola Forenza)

Jiji la Roma linatoa heshima kwa Papa Leo XIV

Dominika tarehe 25 Mei 2025,kabla ya adhimisho la Ekaristi kwa ajili ya kusimikwa kwake katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Yohane wa Laterano,Papa atapokelewa na kutambuliwa na Meya wa Mji wa Roma Bwana Gualtieri chini ya ngazi za Mlima wa Makao makuu ya Manispaa ya Jiji.

Vatican News

Katika Uwanja wa Ara Coeli, chini ya ngazi za kilima cha Manispaa, Papa Leo XIV atapokea heshima kutoka kwa Jiji la Roma kwa mikono ya  Meya wa mji, Bwana  Roberto Gualtieri. Katika taarifa iliyotolewa kutoka Vyombo vya habari Vatican ilitangaza kuwa tukio hilo litafanyika saa 10:15 jioni, Dominika, tarehe 25 Mei, 2025,  siku ambayo Papa Leo XIV ataongoza adhimisho la Ekaristi Takatifu na kusimikwa kwenye Kanisa Kuu la Roma kuwa Askofu wa Roma katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Yohane wa Laterano.

Meya wa mji wa Roma Bwana Roberto Gualtieri
Meya wa mji wa Roma Bwana Roberto Gualtieri   (AFP or licensors)

Katika taarifa hiyo inabainisha kuwa mara baada ya liturujia, Baba Mtakatifu ataonekana kutokea katikati  ya Kanisa Kuu la  Lateranoili kubariki mji wa Roma. Saa 1 jioni, Papa atahamia katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Maria Mkuu kwa muda wa maombi mbele ya Picha ya  Bikira Maria Salus Populi Romani( Afya ya Waroma.)

23 Mei 2025, 09:58