ÐÓMAPµ¼º½

Kutangazwa kwa Mwenyeheri Carlo Acutis na Jubilei ya barubaru  imeahirishwa kutokana na kifo cha Papa. Kutangazwa kwa Mwenyeheri Carlo Acutis na Jubilei ya barubaru imeahirishwa kutokana na kifo cha Papa.  (ANSA)

Utangazaji wa Carlo Acutis kuwa mtakatifu umeahirishwa

Kutokana na kifo cha Papa Francisko,kilichotokea tarehe 21 Aprili,Ofisi ya Waandishi wa Habari ya Vatican imetangaza kuahirishwa kwa sherehe hiyo iliyokuwa imepangwa kufanyika Dominika ya II ya Pasaka tarehe 27 Aprili katika maadhimisho ya Jubilei ya watoto na barubaru.Pia tamasha la muziki kwa ajili ya Jubilei ya watoto tarehe 26 limefutwa.

Vatican News

Katika Dominika  ya pili ya Pasaka, ambayo pia inajulikana kama Dominika ya Huruma ya Mungu, sherehe ya kutangazwa kuwa Mtakatifu kwa mwenyeheri Carlo Acutis iliyokuwa imeratibiwa, imeahirishwa kwa kijana huyo aliyekufa akiwa na umri wa miaka kumi na tano kwa sababu ya ugonjwa wa saratani ya damu mnamo tarehe 12 Oktoba 2006 na kutangazwa mwenyeheri huko Assisi mnamo tarehe 10 Oktoba 2020. Mwili wake umekuwa ukipumzika tangu 2019  katika Kanisa la Mtakatifu Maria Mkuu ( Maria maggiore), Assisi.

Kwa njia hiyo Ofisi ya Waandishi wa Habari ya Vatican imefahamisha kwamba adhimisho la Ekaristi Takatifu na ibada ya kutangazwa  kuwa mtakatifu iliyopangwa kufanyika Dominika katika maadhimisho ya Jubilei ya Vijana, imesitishwa.

Jubilei ya Barubaru

Katika taarifa ya Baraza la Kipapa la Uinjilishaji ilibainisha kwamba  "kwa umoja na watu wote wa Mungu, Kanisa Katoliki na dunia nzima, kwa huzuni tunaungana katika sala kwa ajili ya kuondokewa na Baba Mtakatifu Francisko." Baraza la kipapa pia lilitangaza kwamba "Jubilei  ya Vijana na barubaru imethibitishwa katika mpango wake wa asili. Wakati wa maombi wa "njia ya Msalaba itafanyika Aprili 25: viwanja vya "Majadiliano na jiji". Jumamosi Aprili 26, itakuwa hija za kupita Mlango Mtakatifu na Misa Takatifu, bila kutangazwa kwa Mwenyeheri Carlo Acutis, kwenye Uwanja wa Mtakatifu Petro mnamo Dominika Aprili 27.

Kwa sababu ya muda wa maombolezo, vile vile tamasha la muziki katika (Circo Massimo) jijini lililokuwa limepangwa kufanyika Aprili 26, saa 11 jioni  limefutwa

21 Aprili 2025, 18:37