杏MAP导航

Tafuta

Papa anaendelea na matibabu ya ugonjwa wa mkamba(bronchitis)katika Hosptali ya Agostino Gemelli Roma. Papa anaendelea na matibabu ya ugonjwa wa mkamba(bronchitis)katika Hosptali ya Agostino Gemelli Roma. 

Papa katika hospitali ya Gemelli,maambukizi ya njia ya upumuaji:anaendelea na matibabu

Ofisi ya Vyombo vya Habari vya Vatican inatangaza matokeo ya kwanza ya vipimo vya kitaalamu vilivyofanyika katika Hosptiali alikolazwa tarehe 14 Februari.Papa,ambaye ana homa kidogo, ameanza matibabu kwa dawa.Msemaji mkuu Dk.Bruni alisema: “Papa Francisko ametulia,yuko katika hali nzuri na amesoma baadhi ya magazeti.

Vatican News

Kutokana na kuendelea kuwa na ugonjwa wa mkamba(bronchitis)katika siku za hivi karibuni, Papa Franciskp, aliyelazwa katika hospitali ya Agostino Gemelli, Roma  asubuhi ya leo tarehe 14 Februari 2025, mwishoni mwa mikutano yake iliyokuwa imepangwa “alifanya vipimo vya kitaalam na kuanza matibabu ya dawa katika hospitali.” Haya yaliripotiwa katika taarifa kutoka Ofisi ya Vyombo vya Habari vya Vatican, ikifahamisha kwamba “vipimo vya  kwanza viliyofanywa vilioniesha kuwa ana maambukizi ya njia ya upumuaji.”


Hata hivyo Hali ya kliniki ya Papa “ni njema, anayo homa kidogo,” kwa mujibu wa  maelezo ya Msemaji wa Vyombo vya habari  Dk. Matteo Bruni na kuongeza kwamba " Papa alikuwa mtulivu, mwenye roho tulivu na alikuwa amesoma baadhi ya magazeti.”

14 Februari 2025, 19:00