Papa Francisko hospitalini Gemelli alipata shambulizi la kipekee la kupumua na kupewa gesi
Vatican News
Baba Mtakatifu leo hii lasiri, baada ya asubuhi kutumia tiba mbadala ya mazoezi ya viungo ya kupumua na sala katika Kikanisa, aliwasilisha shambulio la kipekee la kupumua bronchospasm"(Kwikwi),ambalo, hata hivyo, lilisababisha tukio la kutapika kwa kuvuta pumzi na kuzorota kwa ghafla kwa hali yake ya kupumua.
Baba Mtakatifu alipewa mara moja hewa ya mitambo isiyo na uvamizi, na mwitikio ulikuwa mzuri wa kubadilishana gesi. Baba Mtakatifu daima alibaki macho na mwelekeo mzuri, akishirikiana na hali ya matibabu. Kwa hivyo utabiri unabaki kuhifadhiwa. Na asubuhi alipokea Ekaristi.
Haya ndiyo yaliyoripotiwa katika taarifa ya Ofisi ya Vyombo vya habari, Vatican jioni ya leo hii, tarehe 28 Februari 2025, kuhusiana na afya ya Papa Francisko, ambaye amelazwa tangu tarehe 14 Februari 2025 katika Hospitali ya A. Gemelli Roma.