ĐÓMAPµĽş˝

2025.02.01  Wanahija kutoka Jimbo la Sulmona-Valva. 2025.02.01 Wanahija kutoka Jimbo la Sulmona-Valva.  (VATICAN MEDIA Divisione Foto)

Papa asalimia wanahija waliofika ukumbi wa Paulo VI na katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro

Jumamosi tarehe Mosi Februari 2025,Papa Francisko alitoa salamu kwa wanahija kutoka Jimbo Katoliki la Sulmona-Valva),Italia.Na baadaye alikwenda hata Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro kuwasalimia wanahija wengine wa majimbo ya Capua na Caserta huku akiwashukuru uwepo wao na kuwapa baraka zake.

Na Angella Rwezaula - Vatican

Baada ya katekesi yake, tarehe 1 Februari 2025 , akiwageukia waamini na mahujaji waliofika katika Ukumbi wa Paulo VI mjini Vatican Papa Francisko aliwajulisha “kuwasalimia hata washiriki wa Katekesi ya Jubilei waliokuwa katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro mjini Vatican wakifuatilia. Papa alisema kuwa Hawa ni mahujaji kutoka Jimbo Katoliki la Sulmona-Valva) Italia ambapo baadaye alikwenda hata Kanisa Kuu na kuwasalimia huku akiwashukuru uwepo wao na kuwapa baraka zake. Lakini hata hivyo aliomba wasali sala ya Baba Yetu kabla ya kuwazungukia wote.

Wanahija kutoka Jimbo la Sulmona na Valva
Wanahija kutoka Jimbo la Sulmona na Valva   (Vatican Media)
Furaha ya kusalimia Papa
Furaha ya kusalimia Papa   (VATICAN MEDIA Divisione Foto)
Furaha ya bebembelezo la Papa
Furaha ya bebembelezo la Papa   (VATICAN MEDIA Divisione Foto)

Papa hakuishia hapo bali aliongeza: “Mawazo yangu sasa yanakwenda kwenye hija ya Jimbo la Sulmona-Valva, pamoja na Askofu Michele Fusco, na kwa waseminari wa Bergamo. Wapendwa kaka na dada, ninawahimiza kuelewa na kukaribisha zaidi upendo wa Mungu, chanzo na sababu ya furaha yetu ya kweli. Pia ninawasalimu Waseminari wa Bergamo na kuwahimiza daima kumweka Yesu katikati ya maisha yao. Baraka yangu kwa kila mtu!”

Baada ya katekesi Feb 1
01 Februari 2025, 16:10