ĐÓMAPµĽş˝

2023.04.26 Papa Francisko katika sala kwa Mama  Salus populi romani, katika kanisa Kuu la Maria Mkuu. 2023.04.26 Papa Francisko katika sala kwa Mama Salus populi romani, katika kanisa Kuu la Maria Mkuu. 

Papa huko Mtakatifu Maria Mkuu kukabidhi ziara ya Hungaria

Kwa mara ya 106, Papa Fransisko alikwenda katika Kanisa Kuu la Bikira Maria Mkuu kusali mbele ya Picha ya Salus Populi Romani na kuikabidhi hija yake ya tarehe 28-30 Aprili huko Budapest,katikati mwa Ulaya ambapo kama alivyosema katika Sala ya Malkia wa Mbingu:“upepo wa barafu wa vita unaendelea kuvuma.”

Na Angella Rwezaula,- Vatican.

Kama ilivyo kawaida yake, ni kwa mara ya 106 ambayo Baba Mtakatifu Francisko, asubuhi umatano tarehe 26 Aprili 2023 amekwenda katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Maria Mkuu  Roma ili kusali mbele ya picha ya Bikira Maria Afya ya Waroma na kumkabidhi ziara yake ya kitume ya kwenda nchini Hungaria kuanzia tarehe 28 hadi 30 Aprili 2023. Hayo yamethibitishwa kwa waandishi wa habari na msemaji wa vyombo vya habari Vatican.

Pamoja na ulinzi wa Mama Yetu, ikumbukwe kwamba  Papa aliwaomba waamini wote kumsindikiza katika  safari ya karibu huko Hubagaria ma baada ya sala ya  Malkia wa Mbingu Alifanya hivyo Dominika tarehe 23 Aprili iliyopita akikumbusha ulimwengu kwamba kwa siku tatu atasafiri hadi mji mkuu Budapest “kukamilisha safari aliyofanya mwaka wa 2021 kwa Kongamano la Kimataifa la Ekaristi. Safari, ya baba Mtakatifu  daima alisema, ambayo inafanyika katika Ulaya"ambapo pepo za barafu za vita zinaendelea kuvuma, wakati harakati za watu wengi zinaweka masuala ya dharura ya kibinadamu kwenye ajenda. Papa pia alisisitiza kwao anaowatembela kwa upendo ndugu zake na kwa Hungaria Kaka na dada wakiwa na shughuli nyingi za kutayarisha kuwasili kwake: “Ninawashukuru sana kwa hili. Ninaomba kila mtu anisindikize kwa maombi”.

Papa ameombea ziara yake katika picha ya Salus Populi Romani
26 Aprili 2023, 16:35