ÐÓMAPµ¼º½

Padre Paulo Samasumo mwakilishi wa Vatican News katika Ziara ya Papa Francisko nchini Msumbiji akihojiana na  Sr.Olga Massango, yeye akiwa  mmoja wa wajumbe wa Tume ya maandalizi ya hija Padre Paulo Samasumo mwakilishi wa Vatican News katika Ziara ya Papa Francisko nchini Msumbiji akihojiana na Sr.Olga Massango, yeye akiwa mmoja wa wajumbe wa Tume ya maandalizi ya hija 

Hija ya Papa Francisko nchini Msumbiji:Sr.Olga amani bado ni dhaifu!

Sr.Olga Massango wa Shirika la Mtakatifu Paulo huko Msumbiji,katika mahojiano na Padre Samasumo,mwakilishi wa Vatican News nchini Msumbiji ameeleza kuhusu utofauti uliopo wa maandalizi ya hija za kitume kati ya mwaka 1988 na 2019,kuhusu mapapa wawili.Sr.Olga anatarajia watu wa Msumbiji waimarishwe zaidi matumaini na amani ambayo bado ni dhaifu.Nchini Msumbiji watu wote bila kujali dini wamemkarimu Baba Mtakatifu!

Na Sr. Angela Rwezaula- Vatican News

Mwanashirika la Mtakatifu Paulo Nchini Msumbiji, Sr Olga Massango, ambaye wakati wa Ziara ya Kitume ya  Mtakatifu Yohane Paulo II nchini Msumbiji kati ya tarehe 16 na 19 Septemba 1988, alikuwa kijana mtawa na ambaye alihusishwa katika Tume ya maandalizi na kuandaa mahali pa kufikia, kutokana na uwezo wake wa lugha, kwa sababu ya  kuzungumza lugha ya kireno, kifaransa, kisipanyola na kingereza. Na kwa mara nyingine tena hata katika ziara ya Baba Mtakatifu Francisko, Yeye amechaguliwa katika Tume ya maandalizi. Haya ni kwa mujibu wa maelezo ya Padre Paulo Samasumo, mwakilishi wa Vatican News, aliyeko nchini Msumbiji katika ziara hii ya Kitume ya Baba Mtakatifu akiambatana na wengine ambapo amehojiana naye ili kushirikishana uzoefu wake hasa wa kuwa na fursa ya kushiriki katika tume mbili ya kwanza na ya pili  katika matukio ya ujio wa Papa. 

Ziara ya Mtakatifu Yohane Paulo II nchini msumbiji 1988

Akifafanua juu ya mtazamo wake kuhusu ushiriki huo wa kamati mbili za maandalizi Sr. Olga Massango, anasema, kuna utofauti sana, kwani kunako mwaka 1988 Mtakatifu Yohane Paulo II alipokuwa nchini Msumbiji alikuta nchi yote ikiwa imejaa vita ya wenyewe kwa wenye. Serikali ilikuwa ya Kimarx au kikomunisti. Na wakati ule, Vatican ililazimika kuwa na uangalizi wa karibu kuhusu maandalizi hayo yaliyo kuwa yanaandaliwa na watu mahalia. Lakini kinyume na hiyo mandalizi ya mwaka huu, Sr Olga anathibitisha kwamba, tume ya maandalizi mahalia, imetambua nini inapaswa kufanya na kwa maana hiyo hapakuwapo na ulazima wa uangalizi wa karibu kwa upande wa Vatican. Na kama ilivyokuwa hija ya  mtangulizi wake Mtakatifu Yohane Paulo II, hata Baba Mtakatifu Francisko sasa yupo nchini Msumbiji kwa ajili ya kuwatia moyo wa kuwa  na matumaini, amani na kuishi kwa mapatano nchini Msumbiji.

Ziara ya Papa isaidie kuleta ushuhuda mzuri na mfano wa kuigwa nchini Msumbiji

Sr. Olga akiendelea kutazama kwa karibu ziara hii amesema kwamba, hata ziara ya Baba Mtakatifu Francisko ni ya lazima, kwa sababu amani nchini Msumbiji bado ni dhaifu. Iwapo nchini Msubiji watu wataweza kushinda kwa ajili ya amani, nchi itakuwa na ushuhuda mzuri kwa ajili ya nchi nyingie za Afrika kama vile Sudan ya Kusini, amethibitisha Sr. Olga. Aidha Sr, Olga ameshirikisha hata juu ya  matarajio yake kabla ya  mchana wa siku Alhamisi ya tarehe 5 Septemba 2019, mahali ambapo ratiba ya Baba Mtakatifu Francisko ilikuwa ni kukutana na watawa, waseminari na mapadre wa Msumbiji. Kutokana na hili amesema ni matarajio ya kwamba Baba Mtakatifu Francisko anaweza kuwatia moyo hasa watawa ili wasiache utume wa uinjilishaji hata kama wanapata na taaluma za juu kama za ualimu au udaktari. Kwa upande wa mkutano na vijana na Baba Mtakatifu ni matarajio ya Sr Olga juu ya umuhimu wa vijana kwa ajili ya Ekolojia.

Padre Bernardo Suate:ni furaha na chereko kubwa zinazoonekana nchini Msumbiji

Naye  Padre Bernardo Suate, mwakilishi wa Vatican News nchini Msumbiji, katika ziara ya kitume ya Baba Mtakatifu Francisko, wakati wa kuzungumza moja kwa moja na waandishi wa habari Vatican akiwa Msumbiji asubuhi tarehe 5 Septemba 2019, ameelezea kile kinachojiri nchini Msumbiji katika fursa ya ujio wa Baba Mtakatifu tangu alipowasiri katika uwanja wa Maputo tarehe 4 Septemba 2019. Kwa hakika amethibitisha kuwa, ni furaha kwa watu wote, bila kujali dini yoyote. Na zaidi hata katika Luninga ya kitaifa inalezea habari za Baba Mtakatifu katika kipindi hiki cha kihistoria. Kadhalika akifafanua hata juu ya magazeti ndani ya nchi Padre Suate anasema kuwa , karibu ni mahgazeti  yote yametoa kipaumbele cha hija ya Baba Mtakatifu Francisko. Hata hivyo amefurahishwa na habari moja ndani ya gazeti kuhusu bibi mmoja mzee ambaye  siyo mkatoliki na wala mkristo kuthibitisha kwamba, hataki hakose tukio lolote linaloendelea kuhusu  Baba Mtakatifu Francisko nchini humo.

SR OLGA MSUMBIJI
05 Septemba 2019, 13:38