杏MAP导航

Tafuta

Wapalestina wakisubiri kupokea chakula kutoka katika jiko la upendo, katika mji wa Gaza. Wapalestina wakisubiri kupokea chakula kutoka katika jiko la upendo, katika mji wa Gaza. 

Utapiamlo:kijana wa Gaza wa miaka 20 afariki baada ya kuwasili Italiwa kwa matibabu

Mpalestina Marah Abu Zuhri aliyeletwa Italia kati ya tarehe 13 na 14 Agosti 2025 kwa ndege ya serikali ya Italia,lakini hali yake ikionekana kuwa mbaya mara moja alifariki dunia. Waathirika wengine tisa waliuawa katika shambulio kwenye eneo la usambazaji wa misaada ya kibinadamu katika Ukanda huo.Kulingana na UNHCR,Wapalestina wasiopungua 1,760 wameuawa kwa njia hii tangu mwisho wa Mei.

Vatican News

Mwathiriwa wa njaa na utapiamlo, Marah Abu Zuhri, mwanamke wa Kipalestina mwenye umri wa miaka 20 ambaye aliwasili Italia kutoka Ukanda wa Gaza kupata huduma ya matibabu kama sehemu ya operesheni ya kibinadamu, alifariki dunia katika kitengo cha damu cha Hospitali ya Pisa nchini Italia. Alishuka kwa ndege ya serikali ya Italia wakati wa usiku kati ya Agosti 13 na 14 na mara moja alilazwa hospitalini, lakini hali yake mara moja ilionekana kuwa mbaya kwa sababu ya utapiamlo.

Vyakula vikishusha namna hiyo huko Gaza
Vyakula vikishusha namna hiyo huko Gaza

Mwanamke huyo kijana alikuwa amewasili Italia, akifuatana na mama yake, kama sehemu ya operesheni ya kibinadamu, na matokeo ya vipimo kuonesha kuathirika sana na kuzorota kwa kiasi kikubwa, kwa mujibu wa maelezo ya  Hospitali ya Chuo Kikuu cha Pisa. Siku ya tarehe 15  Agosti 2025, baada ya vipimo muhimu vya awali kufanywa na tiba ya kuunga mkono ilianzishwa, alipata shida ya kupumua kwa ghafla na mshtuko wa moyo uliofuata, ambao, kwa bahati mbaya, ulisababisha kifo cha mwanamke huyo kijana.

Gaza, cento Ong contro Israele: basta usare la fame come arma

Wapalestina 1,760 waliuawa wakitafuta msaada tangu Mei

Wakati huo huo, takriban Wapalestina tisa wameuawa na wengine kujeruhiwa,  wakati wa mashambulizi ya Israel kaskazini mwa Ukanda wa Gaza, katika eneo la kusambaza misaada. Shirika la habari la Palestina "Wafa" liliripoti hili, likinukuu vyanzo vya ndani. Zaidi ya Wapalestina 1,760 wameuawa katika Ukanda huo tangu mwishoni mwa Mei, wengi wao chini ya moto wa jeshi la Israel, walipokuwa wakitafuta msaada wa kibinadamu."

Hali ngumu huko Gaza ya kuweza kupata chakula watoto
Hali ngumu huko Gaza ya kuweza kupata chakula watoto

Hayo yameripotiwa na Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa katika maeneo ya Palestina. Kati ya Mei 27 na Agosti 13, Kamishna Mkuu alirekodi angalau "Wapalestina 994 waliuawa walipokuwa wakitafuta msaada karibu na maeneo yanayosimamiwa na Msaada wa Kibinadamu wa Gaza (GHF) na 766 kwenye njia za msafara wa usambazaji," ilisema katika taarifa. "Mauaji mengi haya yalifanywa na jeshi la Israel," shirika la Umoja wa Mataifa linadai.

17 Agosti 2025, 10:30