杏MAP导航

Tafuta

2025.08.22 Papa na Bwana Wavel Ramkalawan, Rais wa Jamhuri ya SheliSheli (Seychelles). 2025.08.22 Papa na Bwana Wavel Ramkalawan, Rais wa Jamhuri ya SheliSheli (Seychelles).  (@Vatican Media)

Papa Leo XIV akutana na Rais wa Jamhuri ya Shelisheli

Ushirikiano na Kanisa mahalia,juu ya ulinzi wa mazingira,afya na elimu:ndizo mada kuu zilizojadiliwa wakati wa mkutano mjini Vatican na Wavel Ramkalawan,Rais wa Jamhuri ya Shelisheli.Majadiliano yaliyofuata katika Sekretarieti ya Vatican pia yalijumuisha kubadilishana mawazo kuhusu masuala ya kikanda na kimataifa,yakionesha umuhimu wa kukuza mazungumzo na ushirikiano kati ya mataifa.

Vatican News

Kwa mujibu wa  taarifa kwa vyombo vya habari kutoka Ofisi ya Waandishi wa Habari ya Vatican  tarehe 22 Agosti 2025 imebanisha kuwa “tarehe 22  Agosti 22025,  Baba Mtakatifu Leo XIV alimpokea na kukutana katika Jumba la  Kitume na Rais wa Jamhuri ya Shelisheli, Bwana Wavel Ramkalawan.

Papa leo na Rais wa Shelisheli
Papa leo na Rais wa Shelisheli   (@Vatican Media)

Baadaye Rais Ramkalawan alikutana na Kardinali Pietro Parolin Katibu Mkuu wa Vatican, akiandamana na Monsinyo Miros?aw Stanis?aw Wachowski, Katibu Msaidizi wa Mahusiano na Mataifa.

Ugeni kutoka Shelisheli
Ugeni kutoka Shelisheli   (@Vatican Media)

Mazingira, afya, elimu, mazungumzo

Wakati wa majadiliano ya ukarimu katika Sekretarieti ya Vatican yalionesha  uhusiano mzuri kati ya Vatican na Shelisheli na mambo mbalimbali ya hali ya kisiasa na kijamii ya nchi yalijadiliwa, hasa ushirikiano na Kanisa la mahalia,  katika nyanja za ulinzi wa mazingira, afya, na elimu, kwa kuzingatia hasa elimu ya vijana wa visiwa hivyo. Mazungumzo yaliendelea kwa kubadilishana mawazo kuhusu masuala ya kikanda na kimataifa, yakisisitiza umuhimu wa kukuza mazungumzo na ushirikiano kati ya mataifa.

Rais wa Shelisheli pamoja na Katibu Mkuu wa Vatican.
Rais wa Shelisheli pamoja na Katibu Mkuu wa Vatican.   (@Vatican Media)

Zawadi kutoka kwa Baba Mtakatifu

Papa alimpatia Rais nakala  msingi inayoonesha fumbo la Taalimungu ya mchoraji Raphael Sanzio inayopatikana katika chumba cha mihuri  katika Makumbusho ya Vatican; mwanamke akiwa amezungukwa na makerubi wawili wenye maandishi "Divinar(um) rer(um) notitia," ikimaanisha taalimungu kama "ufunuo wa mambo." Zawadi zingine kutoka kwa Papa: kitabu cha  Ghorofa ya Watazamaji katika Jumba la Kitume na Ujumbe kwa Siku ya Amani Ulimwenguni kwa mwaka  2025.

Kubadilishana zawadi
Kubadilishana zawadi   (@Vatican Media)

Zawadi kutoka kwa Rais

Rais wa Visiwa vya Shelisheli alimpa Papa mfano mdogo wa mtumbwi wa kawaida wa mbayo wa kuvua samaki kutoka kwenye visiwa.

Kubadilishana zawadi
Kubadilishana zawadi   (@Vatican Media)
Papa na Rais wa Shelisheli
22 Agosti 2025, 16:08