杏MAP导航

Tafuta

Papa amemteua Balozi Mpya wa Vatican nchini Burkina Faso. Papa amemteua Balozi Mpya wa Vatican nchini Burkina Faso. 

Papa Leo XIV amemteua Mons.Eric Soviguidi kuwa Balozi wa Vatican nchini Burkina Faso

Monsinyo Eric Soviguidi,hadi uteuzi huo,alikuwa ni Mwakilishi wa Kudumu wa Vatican katika Mashrika ya Umoja wa Mataifa kwa ajili ya Elimu,Sayansi na Utamaduni na kuinuliwa hadhi ya kuwa na kiti cha Cartenza na Uaskofu mkuu.

Vatican news

Baba Mtakatifu amemtua, Balozi mpya wa Burkina Faso, Mheshimiwa, Monsinyo Eric Soviguidi, ambaye hadi uteuzi huo, alikuwa ni Mwakilishi wa Kudumu wa Vatican katika Mashirika ya Umoja wa Mataifa kwa ajili ya Elimu, Sayansi na Utamaduni, na kumwinua wakati huo huo hadhi ya kuwa na Kiti cha  Cartenza na Uskofu Mkuu.

Wadhifa wake:

Monsinyo Eric Soviguidi alizaliwa huko Abomey nchini Benin kunako tarehe 31 machi 1971. Alipewa daraja la Upadre kunako tarehe 10 Oktoba 1998, kwa ajili ya Jimbo katoliki la Cotonou. Ana shahada ya Sheria za Kanononi za Kanisa.

Alijiunga katika huduma ya kidiplomasia ya Vatican kuna tarehe 1 Julai 2005 na kutoa huduma kwenye Balozi za Vatican kwa nchi kadhaa: Haiti, Ghana, Tanzania, Guatemala, Katika Kitengo Sekretarieti ya Vatican cha Mahusiano na Nchi na Mashirika ya Kimataifa  na hatimaye alikuwa katika Mashirika ya Umoja wa Mataifa kwa ajili ya Elimu, Sayansi na Utamaduni kama Mwakilishi wa Kudumu wa Vatican. Anazungumza pamoja na kuzungumza kifaransa, pia ni kiingereza, kiitaliano na kispanyola.

15 Agosti 2025, 12:28