杏MAP导航

Tafuta

Baba Mtakatifu Leo XIV Jumamosi tarehe 28 Juni 2025 amekutana na kuzungumza na Rais Teodoro Obiang Nguema Mbasogo wa Guinea ya Ikweta, Baba Mtakatifu Leo XIV Jumamosi tarehe 28 Juni 2025 amekutana na kuzungumza na Rais Teodoro Obiang Nguema Mbasogo wa Guinea ya Ikweta,   (ANSA)

Rais Carlos Manuel Vila Nova Akutana na Papa Leo XIV Mjini Vatican

. Baba Mtakatifu Leo XIV katika mazungumzo na mgeni wake, wamepongeza uhusiano mzuri wa kidiplomasia uliopo kati ya nchi hizi mbili, na baadaye wakajielekeza katika masuala ya kisiasa na kiuchumi, sanjari na mchango wa Kanisa Katoliki katika ustawi, maendeleo na mafao ya wengi, hususan katika huduma ya afya, elimu; malezi na majiundo kwa vijana wa kizazi kipya. Wamebadilishana mawazo kuhusu umuhimu wa majadiliano na ushirikiano wa Kimataifa.

Na Padre Richard A. Mjigwa, C.PP.S. – Vatican.

Baba Mtakatifu Leo XIV Jumatatu tarehe 30 Juni 2025 amekutana na kuzungumza na Rais Carlos Manuel Vila Nova wa Sao Tome na Prince na baadaye akakutana na kuzungumza na Askofu mkuu Paul Richard Gallagher, Katibu mkuu wa Mambo ya Nchi za Nje, Ushirikiano na Mashirika ya Kimataifa. Baba Mtakatifu Leo XIV katika mazungumzo na mgeni wake, wamepongeza uhusiano mzuri wa kidiplomasia uliopo kati ya nchi hizi mbili, na baadaye wakajielekeza katika masuala ya kisiasa na kiuchumi, sanjari na mchango wa Kanisa Katoliki katika ustawi, maendeleo na mafao ya wengi, hususan katika huduma ya afya, elimu; malezi na majiundo kwa vijana wa kizazi kipya.

Raais Carlos Manuel Vila Nova amekutana na Papa Leo XIV mjini Vatican
Raais Carlos Manuel Vila Nova amekutana na Papa Leo XIV mjini Vatican   (ANSA)

Katika mazungumzo yao, wamebadilishana mawazo kuhusu mada mbalimbali za Kikanda na Kimataifa, kwa kukazia umuhimu wa Jumuiya ya Kimataifa kuendelea kujikita katika mchakato wa majadiliano katika ukweli na uwazi pamoja na ushirikiano wa Kimataifa kwa ajili ya ustawi, maendeleo na mafao ya wengi.

Sao Tome

 

30 Juni 2025, 14:40