杏MAP导航

Tafuta

2025.06.24  Padre Francesco Ielpo(OFM) Msimamizi mpya wa Nchi Takatifu. 2025.06.24 Padre Francesco Ielpo(OFM) Msimamizi mpya wa Nchi Takatifu. 

Padre Francesco Ielpo(OFM) ni Msimamizi mpya wa Nchi Takatifu

Papa Leo XIV amemteua Padre Francesco Ielpo(OFM kuwa Msimamizi wa Nchi Takatatifu na Mkuu wa Conventi ya Mlima Sion.Habari hizo zilitangazwa asubuhi ya Jumanne,Juni 24,kwa barua rasmi iliyotumwa na Mkuu wa Shirika la Wafransiskani,Ndugu Massimo Fusarelli(OFM).Ndugu Francesco Ielpo,alizaliwa huko Lauria(jimbo la Potenza)mnamo tarehe 18 Mei 1970.

Na Angella Rwezaula – Vatican.

Baba Mtakatifu Leo XIV amemteua Padre Francesco Ielpo, O.F.M., kuwa Msimamizi wa Nchi Takatatifu na Mkuu wa Conventi ya Mlima Sion. Uteuzi wake unathibitisha kumaliza muda wake Padre Francesco Patton ambaye amekuwa msimamizi wa Nchi Takatifu tangu mwaka 2016, akiwa mkuu wa Shirila la  Wafransiskani walioko Israel, Palestina, Syria, Jordan, Lebanon, Cyprus na Rhodes. Ni katika habari iliyowasilishwa asubuhi ya Jumanne  tarehe 24 Juni 2025, kwa barua rasmi iliyotumwa na Mkuu wa Shirika la Wafransiskani, Fra Massimo Fusarelli (OFM).

Wasifu wake(CV)

Padre Francesco Ielpo, ni mzaliwa wa italia huko  Lauria  Jimbo la Potenza(PZ) tarehe 18 Mei 1970. Alijiunga kwa dhati katika Shirika la  Wafransiskani la Ndugu Wadogo mnamo mwaka 1998; wakati mwaka 2000 alipewa daraja la Upadre. Katika utume wake ameshikilia nyadhifa mbalimbali kama vile: Mwalimu wa Dini (1994-2010); Mkuu wa Taasisi ya Franciscanum  ya Luzzago huko Brescia (tangu 2000); Mjumbe wa Baraza la Kitaifa la FIDAE (Shirikisho la Taasisi za Shughuli za Kielimu) (2006-2010); Mkuu wa Kanda ya Lombardia (2007-2010); Paroko wa Mtakatifu Antonio wa Padova huko Varese (2010-2013).

Padre Ielpo (OFM)
Padre Ielpo (OFM)

Kuanzia Septemba 2013 hadi 2016 alikuwa Kamishna wa Nchi Takatifu ya Lombardia, akiendelea na jukumu hilo kutoka 2016 hadi 2023 kwa Kanda ya  Kaskazini mwa Italia. Tangu 2014 amekuwa mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya Chama cha Pro Terra Sancta. Na wakati huo tangu 2022  Rais wa Mfuko wa Nchi Takatifu, Mjumbe wa Nchi Takatifu kwa Italia, Mjumbe Mkuu wa urekebishaji wa Kanda za Campania, Basilicata na Calabria.

Padre Ielpo (OFM)
Padre Ielpo (OFM)
24 Juni 2025, 15:56