杏MAP导航

Tafuta

Deni la kiikolojia na linahusu nini hasa?Ni kuakisi jinsi uchumi ulioendelea zaidi kiviwanda na kuwa wasanifu wakuu wa shida ya tabianchi,pia kutokana na unyonyaji wa maliasili za nchi masikini. Deni la kiikolojia na linahusu nini hasa?Ni kuakisi jinsi uchumi ulioendelea zaidi kiviwanda na kuwa wasanifu wakuu wa shida ya tabianchi,pia kutokana na unyonyaji wa maliasili za nchi masikini. 

Jubilei 2025:Ondoleo la madeni kiekolojia

Baraza la Kipapa kwa ajili ya kuhamasisha Maendeleo Fungamani ya Binadamu imechapisha dokezo la mada kuhusu ondoleo la deni la kiikolojia,(kama lengo la kuanzia tena katika mwaka huu wa matumaini wa Jubilei 2025.Kufutwa kwa deni la kifedha ambalo linazielemea nchi maskini zaidi hakupaswi kuonekana kama ishara ya mshikamano na ukarimu tu bali kama ishara ya haki ya kurejesha.

Vatican News

Ujumbe wa mada  ya"Jubilei 2025: msamaha wa deni la ikolojia", ”, uliotiwa saini na Baraza la Kipapa kwa ajili ya Kuhamasisha Maendeleo Fungamani ya Binadamu ulichapishwa tarehe 24 Juni 2025, ambao unaweza kupakuliwa katika lugha 5. Hati hiyo inaelezea jinsi ambavyo deni la kifedha na deni la kiikolojia leo hii linawakilisha pande mbili za sarafu moja. Wakati kwa upande mmoja, nchi zinazoendelea zimelemewa leo na deni la kiuchumi ambalo lina mizizi ya mbali na kwamba janga hilo limezidi kuwa mbaya, pia zinakabiliwa na athari mbaya zaidi za mzozo wa tabianchi, licha ya kutokuwa miongoni mwa wahusika wakuu wa hilo.

Kufutwa kwa deni la nchi masikini aidi ni ishara ya haki

Lakini nini maana ya deni la kiikolojia hasa? Ujumbe huo unaakisi jinsi uchumi ulioendelea zaidi kiviwanda, ndio wasanifu wakuu wa shida ya tabianchi, pia kutokana na unyonyaji wa maliasili za nchi masikini, ambazo hata hivyo hazina "rasilimali za kiuchumi na miundombinu zinazohitajika kurekebisha au kuguswa," na hivyo kuzidisha mzozo wa kiuchumi na shida ya mazingira, na matokeo yasiyoweza kuepukika kwa maendeleo ya watu. Kwa mtazamo huu, kufutwa kwa deni la kifedha ambalo linazielemea nchi maskini zaidi hakupaswi kuonekana kama ishara ya mshikamano na ukarimu, bali kama ishara ya haki ya kurejesha.

Mpango huu ni ujenzi mpya wa muungano kati ya watu 

Mpango kama huo hautakuwa kitendo cha kuadhibu, lakini badala yake ni viaticum kwa ujenzi wa muungano mpya kati ya watu, ambao una haki ya kijamii na kujali uumbaji moyoni. Ukisukumwa na Jubilei ya Matumaini na kuongozwa na maneno ya Baba Mtakatifu Leo XIV,  Vatican  kwa  kanuni za Mafundisho Jamii, inapyaisha dhamira yake ya kichungaji kwa haki ya kiikolojia, kijamii na kimazingira. Kwa sababu hiyo, waraka unaalika Makanisa mahalia kukuza, katika mazingira tofauti ya kijamii, uwongofu muhimu wa ikolojia, "binafsi na jumuiya".

Ikumbukwe kwamba kazi hii imetumia uchambuzi wa pamoja wa CAFOD() Shirika la misaada la kimaendeleo la Kikatoliki, Mtandao wa Haki na Ikolojia wa Kijesuit - Afrika (JENA) na  , ambao ulipelekea kuchapishwa kwa waraka wa Kuziba Mgawanyiko wa Kaskazini-Kusini: Wajibu wa Pamoja wa Haki ya Kiuchumi na Ikolojia.

25 Juni 2025, 11:57