杏MAP导航

Tafuta

2025.05.03 Constantine Chiwenga, Makamu Rais wa  Zimbabwe mjini Vatican. 2025.05.03 Constantine Chiwenga, Makamu Rais wa Zimbabwe mjini Vatican.  (@VATICAN MEDIA)

Gallagher akutana na makamu rais wa Zimbabwe

Mazungumzo ya hali ya kisiasa na kijamii na kiuchumi yalikuwa katikati ya mkutano mjini Vatican kati ya Jenerali Constantino Guveya Dominic Nyikadzino Chiwenga na Katibu wa Vatican wa Mahusiano na Mataifa na Mashirika ya Kimataifa.

Vatican News

Katika taarifa tunayosoma kutoka katika Ofisi ya vyombo vya habari vya Vatican imerejea juu ya mkutano wa asubuhi ya tarehe 3 Mei 2025 mjini Vatican, kati ya Jenerali Constantino Guveya Dominic Nyikadzino Chiwenga, makamu wa rais wa nchi ya Zimbabwe  na Askofu Mkuu Paul Richard Gallagher, Katibu wa Vatican wa Mahusiano na Mataifa na Mashirika ya Kimataifa kwamba: “Wakati wa majadiliano ya dhati, uhusiano mzuri kati ya Vatican  na Jamhuri ya Zimbabwe ulibainishwa.”

Makamu rais wa Zimbabwe na Askofu Mkuu Gallagher
Makamu rais wa Zimbabwe na Askofu Mkuu Gallagher   (@VATICAN MEDIA)

Mkutano huo pia ulijadili baadhi ya vipengele vya hali ya kisiasa na kijamii na kiuchumi ya nchi, hasa kuhusu ushirikiano na Kanisa mahalia katika nyanja ya elimu na afya. Kulikuwa na mabadilishano ya maoni pia kuhusu masuala ya kikanda na kimataifa, yakionesha umuhimu wa kukuza mazungumzo na maridhiano kati ya watu.

Makamu Rais wa Zimbabwe na Askofu Mkuu Gallagher
Makamu Rais wa Zimbabwe na Askofu Mkuu Gallagher   (@VATICAN MEDIA)
Gallagher na makamu rais wa Zimbabwe
03 Mei 2025, 12:32