杏MAP导航

Tafuta

Moja ya mikutano ya Papa na Mabalozi wa Kitume wa Vatican. Moja ya mikutano ya Papa na Mabalozi wa Kitume wa Vatican. 

Papa afanya Teuzi za Mabalozi wa kitume wa Vatican kwa ajili ya nchi mbali mbali

Papa Jumamosi tarehe 12 Aprili 2025 amefanya teuzi za mabalozi kwa visiwa vya Kook huko Kiribati na visiwa vya Marshall,huko Samoa na Nauru,Askofu Mkuu Gábor Pintér;Balozi wa kitume wa Vatican kwa ajili ya Nchi za Chini,Askofu Mkuu Jean-Marie Speich na hatimaye amemteua Balozi wa Kitume wa Vatican nchini Ethiopia,Askofu Mkuu Brian Udaigwe.

Vatican News

Baba Mtakatifu Francisko,Jumamosi tarehe 12 Aprili 2025 amefanya teuzi mbali mbali katika matukio na  ambapo ni pamoja na mabalozi wa Vatican kwa ajili ya nchi kadhaa: amemteua Balozi wa kitume wa Vatican kwa ajili ya visiwa vya Cook, Kiribati, na visiwa vya Marshall,huko  Samoa na huko Nauru Askofu Mkuu Gábor Pintér, Mwenye makao yake Velebusdo, ambaye ni Balozi wa Kitume wa  Vatican huko New Zeland, Fiji, Palau, na Nchi za Shirikisho la Micronesia na Vanuatu.

Baba Mtakatifu aidha amemteua Balozi wa kitume wa Vatican kwa ajili ya Nchi za Chini , Askofu Mkuu Jean-Marie Speich, mwenye makao yake Sulci, hadi uteuzi huo alikuwa ni Balozi wa Vatican huko  nchini Slovenia na Mwakilishi wa Kitume wa Vatican huko  Kosovo.  Baba Mtakatifu hatimaye amemteua, Balozi wa Kitume wa Vatican nchini Ethiopia, Askofu Mkuu Brian Udaigwe, mwenye makao  yake  Suelli, hadi uteuzi huo alikuwa ni Balozi wa Vatican nchini Sri Lanka.

Uteuzi wa Papa wa Mabalozi

 

12 Aprili 2025, 16:34