杏MAP导航

Tafuta

2025.04.05 Jubilei ya wagonjwa na Ulimwengu wa kiafya. 2025.04.05 Jubilei ya wagonjwa na Ulimwengu wa kiafya.  (Vatican Media)

Mlango Mtakatifu wa Wafamasia,Madaktari na Wafanyakazi wa Afya

Hija ya Jubilei ya jumuiya ya wafanyakazi wa Famasi ya Vatican na Kurugenzi ya Afya na Usafi ndani ya Jubilei ya Wagonjwa na wahudumu wa kiafya:Mkurugenzi Arcangeli wa Dsi: "Ni uzoefu wa maombi ya pamoja na walio dhaifu zaidi."Kutoka kwa mfamasi Ndugu Binish Mulackal:"tiba haitokani na dawa tu bali,zaidi ya yote,kwa kusikiliza na kutoa tabasamu letu kwa wagonjwa"

Na Fabrizio Peloni – Vatican.

Huku miale ya kwanza ya jua ikianza kuchomoza kupitia Uwanja wa Pia, Karibu na Jengo la Baraza la Kipapa la Mawasiliano na kufukuza ukungu usio wa kawaida uliokuwa umeifunika jiji la Roma, ilikuwa jumuiya za kazi za Famasi ya Vatican na Kurugenzi ya Afya na Usafi (Dsi) ya mji wa  Vatican ili  kuzindua, Jumamosi tarehe 5 Aprili 2025 mfululizo mrefu wa maandamano ambayo yalivuka Mlango Mtakatifu wa Kanisa Kuu la Vatican kwa ajili ya  Jubilei ya Wagonjwa na Ulimwengu wa Kiafya. Wafanyakazi wa vyombo hivyo  viwili vya Vatican walitumia fursa ya ukaribu wa maeneo yao ya kazi na Kanisa kuu la Mtakatifu Petro na kuwa miongoni mwa watu wa kwanza kufika mahali pa kuanzia ambapo maandamano ya sala yalipitia (Via della Conciliazione), njia ya Conciliazione.

Jubilei ya wagonjwa na Ulimwengu wa kiafya
Jubilei ya wagonjwa na Ulimwengu wa kiafya   (Vatican Media)

Aliyeongoza wajumbe hao - ambao Dominika waweze kushiriki  kwa wingi zaidi katika Misa ya kuhitimisha Jubilei ya kitengo hicho - alikuwa mkurugenzi wa Famasia ya Vatican Ndugu Thomas Binish Mulackal, mratibu wa mpango huo, pamoja na Profesa Andrea Arcangeli na Dk. Luigi Carbone,  mkurugenzi na makamu mkurugenzi wa DSI. Mtawa wa Kihindi wa Shirika la Hospitali, la Mtakatifu Yohane wa Mungu (Fatebenefratelli) alisisitiza "uzuri wa kuanza siku kama nyingine nyingi kwa njia hiyo, ambayo ilitufanya turudi mahali pa kazi na mioyo yenye amani na iliyojaa matumaini.” Akikumbuka utume wa hali ya juu "uliokabidhiwa na Mungu kwa wafanyakazi wa afya, kuhusiana na dhana kwamba tumaini halikatishi tamaa", alisema kuwa "kwetu hii inamaanisha kuwa tiba haitokani na dawa tu, bali pia na zaidi ya yote, kwa kusikiliza na kutoa tabasamu letu kwa wale watu ambao wanapaswa kukabiliana na ugonjwa kila siku".

Jubilei ya wagonjwa na Ulimwengu wa kiafya
Jubilei ya wagonjwa na Ulimwengu wa kiafya   (Vatican Media)

“Kuvuka Kizingiti mlango Mtakatifu kwa pamoja ilikuwa uzoefu mkubwa, ingawa mfupi, wa maombi ya pamoja kwa walio dhaifu zaidi, na wale ambao wamekusudiwa kuwatazama wagonjwa kitaaluma," Profesa Arcangeli alisema katika suala hili. Kushiriki nafasi sawa "kwenye njia ambayo ilituleta sisi na wenzetu kwenye Mlango Mtakatifu, ilikuwa uzoefu wa nguvu kutoka kwa mtazamo wa kiroho, na tuna hakika kwamba itaturuhusu kutoa huduma bora zaidi ya utunzaji kwa wengine ambao wanajikuta katika hali dhaifu", walitoa maoni Alessandra Ottavianelli na Elena Fontana, kabla ya kurudi nyuma ya dawati la  Duka la dawa wakiwa wamevaa makoti yao meupe.

06 Aprili 2025, 09:59