杏MAP导航

Tafuta

Kumbukizi ya miaka 20 tangu kifo cha Papa Yohane Paulo II. Kumbukizi ya miaka 20 tangu kifo cha Papa Yohane Paulo II.  (VATICAN MEDIA Divisione Foto)

Maelfu ya watu wameshiriki Mkesha wa miaka 20 tangu kifo cha Yohane Paulo II

Leo tunashukuru kwa utambuzi wa yote ambayo Yohane Paulo II alifanya.Tunashuku na tunataka kukumbuka tukio hili,hasa tunataka kurudi katika mafundisho yake.Alithibitisha hayo Askofu Mkuu Tadeusz Wojda,Rais wa Baraza Katoliki la Maaskofu Katoliki la Poland,ambaye aliongoza mkesha wa sala mjini Vatican Aprili 2 katika kumbukizi ya miaka 20 tangu kifo cha Mtakatifu Yohane Paulo II.

Padre Pawe? Rytel-Andrianik na  Artur Hanula - Vatican.

"Tunakumbuka wakati huo wakati watu walipiga magoti hapa kwenye uwanja huu. Wengine walikuwa wakilia, wengine walikuwa wakishangaa kwa nini ameondoka, kwa sababu ilionekana kuwa angeendelea kukaa nasi milele," alisema hayo  Askofu Mkuu Tadeusz Wojda akikumbuka matukio ya miaka 20 iliyopita. "Leo tunakumbuka tukio hili la kumshukuru Mungu kwa upapa huu mkuu na mkuu sana. Ni mojawapo ya matukio makuu zaidi katika historia ya upapa," aliongeza. Kielelezo katika kumwiga Kristo na kielelezo cha uhodari kama vile Mkuu wa Kanisa la Gdańsk alivyokazia, “Yohane Paulo wa Pili, akiwa mshirika wetu mkuu, alituacha sana, na zaidi ya yote alituonesha njia ya kwenda kwa Kristo” na jinsi ya kutembea pamoja na Yesu katika maisha ya kila siku, licha ya dhiki, kuwatumikia wengine. Alisisitiza hayo katika mkesha wa usiku tarehe 2 Aprili 2025 katika Uwanja wa Mtakatifu Petro mjini Vatican, kukumbuka kifo cha Mtakatifu Yohane II kilichokea miaka ishirini iliyopita. Askofu Mkuu Wojda alisema kuwa: “Alikuwa mtu wa sala, mtu wa upendo, mtu wa huduma ya daima kwa wengine,” Mtakatifu Yohane Paulo wa  II pia alikuwa ni  kielelezo cha ujasiri. "Katika ulimwengu wa leo, wakati mwingine inaonekana kuwa ngumu sana kukiri imani yetu. Tunakosa ujasiri, tunakosa nguvu. Wakati mwingine raha za maisha, wakati mwingine masuala mengine hurahisisha sana mtu kumsahau Mungu, alisema Rais wa Baraza la Maaskofu wa Poland. “Na hii ndiyo sababu ni muhimu kurudi kwa Papa Yohane Paulo II sio kama hisia, lakini zaidi ya yote kama mafundisho.

Shukrani kutoka kwa Mkuu wa Kanisa katoliki la Poland wakati wa misa katika Kanisa kuu la Mt. Petro
Shukrani kutoka kwa Mkuu wa Kanisa katoliki la Poland wakati wa misa katika Kanisa kuu la Mt. Petro   (VATICAN MEDIA Divisione Foto)

Sala kwa ajili ya Amani na kwa ajili ya Baba Mtakatifu Francisko

Washiriki wa mkesha huo waliombea amani duniani, hasa nchini Ukraine, Nchi Takatifu na nchi zote za Afrika."Tunataka pia kumwomba Papa Francisko afya, ili aweze kurejesha nguvu zake na kuendelea kuliongoza Kanisa letu," Askofu Mkuu Wojda alihimiza. Pia aliomba kuombea familia na kwa sababu "tukiungwa mkono na mafundisho ya Yohane Paulo II, tunajua jinsi ya kuchagua yaliyo ya kweli, tunajua jinsi ya daima kusimama upande wa neno la Mungu na mapenzi ya Mungu. Kwa hili tunamwomba Mtakatifu Yohane Paulo II pia kwa ajili ya nchi yetu, ambayo pia iko katika shida".

Washiriki wa mkesha katika Uwanja wa Mtakatifu Petro

Washiriki elfu kadhaa Wakazi wa Roma na wawakilishi wa uhamiaji wa Poland walikusanyika kwa wingi kwenye mkesha huo katika Uwanja wa Mtakatifu Petro.  Tafakari wakati wa sala ya rozari iliongozwa na na kuwa na nukuu kutoka kwa mafundisho ya Mtakatifu Yohane Paulo wa Pili. Tukio hilo lilihudhuriwa, miongoni mwa mengine, na Balozi wa Jamhuri ya Poland anayewakilisha nchi yake mjini Vatican, Bwana Adam Kwiatkowski, Balozi Mdogo wa Roma Bartosz Skwarczyński na Maaskofu wa Poland: Askofu Mkuu Tadeusz Wojda, Askofu Mkuu Stanis?aw Budzik, Askofu Mkuu Wiktor Skworc na Askofu Artur Miziński.

Waamini wa Polan katika mavazi ya kitaifa kuadhimisha misa Aprili 2
Waamini wa Polan katika mavazi ya kitaifa kuadhimisha misa Aprili 2   (VATICAN MEDIA Divisione Foto)

Katika mkesha huo pia alishiriki Profesa Miros?aw Kalinowski, Gambera wa Chuo Kikuu cha Kikatoliki cha Yohane  Paulo  II huko Lublin, Poland. Mkutano wa maombi uliandaliwa kwa ushirikiano wa  Ubalozi na Shirika la Mtakatifu Stanis?aw, Bikira na Shahidi wa Roma, Ofisi ya Huduma ya Kichungaji ya Watu wa Kaskazi  wanaokusanyika kwenye Patakatifu pa Mama Yetu wa Msaada wa Kudumu kwenye Njia ya Merulana Roma na katika Kanisa la Mtakatifu Nikolai huko Ostia, pamoja na  Mfuko wa  Vatican wa Mtakatifu Yohane Paulo wa Pili. Kwaya iliyoongoza  ilikuwa ni ya “Gaudium Poloniae” ya kanisa la Mtakatifu  Stanis?ao, Roma.

03 Aprili 2025, 10:36