杏MAP导航

Tafuta

2025.03.28 Rais wa Jamhuri ya Poland Bwana Andrzej Duda na Kardinali Parolin, Katibu wa Vatican. 2025.03.28 Rais wa Jamhuri ya Poland Bwana Andrzej Duda na Kardinali Parolin, Katibu wa Vatican.  (VATICAN MEDIA Divisione Foto)

Rais wa Poland Andrzej Duda,akutana na Katibu wa Vatican

Mazungumzo ya kina katika kuelekea kumbukizi ya miaka 20 ya kifo cha Mtakatifu Yohane Paulo II na milenia ya kutawazwa kwa Mfalme wa kwanza wa Poland, masuala ya kimataifa kwa kuzingatia vita nchini Ukraine na usalama barani Ulaya yalikuwa ni mazungumzo kati ya Rais wa Jamhuri ya Poland,Bwana Duda na Sekretarieti ya Vatican,Jumamosi asubuhi,Machi 28.

Vatican News

Ijumaa asubuhi tarehe 28 Machi 2025, Rais wa Jamhuri ya Poland, Bwana Andrzej Duda, alipokelewa na Katibu wa Vatican, Kardinali Pietro Parolin, akisindikizana na Monsinyo Miros?aw Wachowski, Katibu Msaidizi  wa Vatican kwa ajili ya Mahusiano na Mataifa.

Masuala ya kikanda na kimataifa

Kwa mujibu wa taarifa kutoka Ofisi ya Vyombo vya habari Vatican, ilibainisha kuwa kulikuwa na Mazungumzo ya kina yalifanyika katika kuelekea kumbukumbu ya miaka 20 tangu kifo cha Mtakatifu Yohane Paulo II na katika kuelekea milenia ya kutawazwa kwa Mfalme wa kwanza wa Poland, Boles?aw Chrobry. Baadhi ya mada zenye maslahi kwa pande zote mbili zilijadiliwa. Baadaye, lengo lilikuwa katika masuala ya sasa ya kimataifa, kwa kuzingatia hasa vita vya Ukraine na usalama na amani katika Ulaya.

Rais na Ujumbe wake akiwa na sekretarieti ya Vatican
Rais na Ujumbe wake akiwa na sekretarieti ya Vatican   (VATICAN MEDIA Divisione Foto)
Kardinali Parolin akutana na Rais wa Poland
28 Machi 2025, 14:53