杏MAP导航

Tafuta

Papa Francisko Feb 14, alikutana  na Waziri Mkuu wa Slovakia. Papa Francisko Feb 14, alikutana na Waziri Mkuu wa Slovakia.  (Vatican Media)

Papa akutana na Fico,Waziri Mkuu wa Slovakia

Waziri Mkuu,akiwa na ujumbe,alipokelewa na Papa katika Nyumba ya Mtakatifu Marta mjini Vatican,Ijumaa tarehe 14 Februari 2025.Katika mazungumzo na Sekretarieti ya Vatican kukosekana kwa utulivu nchini Ukraine na matarajio ya amani,juu ya maelewano dhaifu katika Israeli na Palestina na juu ya dharura ya kibinadamu huko Gaza,vilizungumzwa.

Vatican News

Mkutano kati ya Baba Mtakatifu Francisko na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Slovakia,Bwana Robert Fico,Ijuma tarehe 14 Februari 2025 yalichukua muda wa nusu saa, kuanzia saa 9 hadi 9:30, aliyekaribishwa katika ukumbi wa Nyumba ya Mtakatifu  Marta mjini Vatican mahali ambapo Baba Mtakatifu Francisko amekuwa akiendelea na shughuli zake kutokana na ugonjwa wa mkamba ambao amekuwa akiugua kwa siku kadhaa. Aliyeambatana na Waziri Mkuu ni ujumbe wa wajumbe sita, akiwemo mama yake mzazi mwenye umri wa miaka 83, kama ilivyotangazwa na Fico mwenyewe tarehe 13 Februari  kupitia akaunti zake za mitandao ya kijamii.

Papa akutana na Waziri wa Slovakia
Papa akutana na Waziri wa Slovakia

Mara baada ya hapo, mkuu wa serikali ya Bratislava alihamia katika Jumba  jingine la Vatican ili kufanya  mkutano  na Sekretarieti ya  ya Vatican kwa hiyo na  Kardinali Pietro Parolin, akiambatana na Monsinyo Miros?aw Wachowski, Katibu Msaidizi wa  Vatican wa Mahusiano na Mataifa. Taarifa ya Ofisi ya Vyombovya habari inabainisha kuwa  Wakati wa majadiliano kulikuwapo na kulithibitishwa tena shukrani kwa pande zote juu ya uhusiano thabiti wa nchi mbili na kujitolea upya kwa pamoja kuhusiana na masuala ya kijamii. Katika muktadha huo, umakini maalum ulipewa kwa suala la kianthropolojia na masuala yanayohusiana na familia na elimu. Hali halisi ya kimataifa pia ilichunguzwa kwa kina, huku  ikizingatia kukosekana kwa utulivu nchini Ukraine na matarajio ya amani, na vile vile juu ya makubaliano dhaifu ya Israeli na Palestina na dharuraaya kibinadamu huko Gaza.

Zawadi

Mwishoni mwa mazungumzo ya faragha, Papa, wakati wa kubadilishana zawadi za kiutamaduni, alimpatia Waziri Mkuu kazi ya kisanii ya Udongo wa Mfinyanzi inayoitwa "Huruma na Upendo", pamoja na hati za Papa, Ujumbe wa Amani wa mwaka huu 2025, Kitabu cha Kuteswa kwa Ukweli, cha Wakatoliki wa Uigiriki nyuma ya Pazia la Chuma" na albam  ya picha za rangi iliyochapishwa na LEV, matokeo ya mpango wa utafiti wa Taasisi ya Historia ya Kanisa ya Chuo Kikuu katoliki cha Kiukraine kuhusu maisha ya fumbo la  Kanisa Katoliki la Kigiriki la Kiukraine  na  urithi wafiadini. Waziri Fico alijibu kwa kazi ya shaba inayowaonesha Watakatifu Cyril na Methodius, Maaskofu wasimamizi wa Bara la Ulaya ambao sikukuu yao inaadhimishwa kila ifikapo tarehe 14 Februari, na mchoro wa msanii wa Slovakia anayeonesha Malaika mlinzi.

Shambulio la kupigwa risasi 2024

Hata hivyo katika ratiba ya mkuu wa serikali ya Bratislava atatembelea Chuo cha Kipapa cha Watakatifu wa Kislovakia Cyril na Methodius kilicho roma tarehe 14 Februari 2025. Mwaka 2024, mwezi wa Mei, Waziri  Fico alikuwa mwathirika wa jaribio la mauaji, baada ya mkutano huko Handlova, alipigwa risasi kwenye kifua, tumbo na kiungo kimojawapo. Shambulio ambalo Papa mwenyewe pia alilikumbuka katika hotuba yake kwa bodi za wanadiplomasia wa Vatican kunako  Januari iliyopita, huku akionesha kama mfano wa kusikitisha wa hali ya mashaka inayotokana na habari za uwongo ambazo huchochea chuki na kuhatarisha kuishi kwa raia na utulivu wa mataifa yote.

Papa na waziri Mkuu Fico
14 Februari 2025, 17:00