杏MAP导航

Tafuta

Waziri Mkuu wa Ufaransa Bayrou akutana na Katibu wa Vatican, Kardinali Pietro Parolin. Waziri Mkuu wa Ufaransa Bayrou akutana na Katibu wa Vatican, Kardinali Pietro Parolin.  (ANSA)

Kardinali Parolin atembelea Paris na kukutana na Waziri Mkuu Bayrou

Katibu wa Vatican katika mkuu wa Ufaransa Januari 15 na 16 kushiriki katika mkutano ulioandaliwa huko Quai d'Orsay kwa ajili ya hafla ya kuadhimisha miaka 100 ya kubadilishana barua kati ya Waziri Mkuu wa wakati huo,Poincaré na Balozi wa Vatican Cerretti kuhusu vyama vya majimbo.Kardinali aliyepokelewa na Matignon Waziri Mkuu tarehe 15 Januari pia kuwa na mazungumzo na Mawaziri wa Mambo ya Ndani na Mambo ya Nje yaliyopangwa.

Vatican News

Kardinali Pietro Parolin, Katibu wa Vatican yuko nchini Ufaransa ili  kushiriki Kongamano la Quai d'Orsay huko Paris lililotolewa kwa ajili ya kumbukizi ya ubadilishanaji wa barua uliofanyika miaka mia moja iliyopita (11 - 17 Januari 1924) kati ya kipindi cha utume wa Balozi wa Vatican nchini Ufaransa, Monsinyo Bonaventura Cerretti, ambaye angekuwa Kardinali baadaye mwaka uliofuata 1925,na Waziri Mkuu, Raymond Poincaré, Rais wa zamani wa Jamhuri hiyo.

Baraza la nchi ya Ufaransa linayachukulia maandishi hayo kama makubaliano ya kimataifa yanayofangamanisha Ufaransa na Vatican na kuruhusu kuanzishwa kwa chama cha majimbo katika kila Jimbo na  hivyo kurekebisha ombwe la kisheria lililoanzishwa na sheria ya 1905 ya kutenganisha Makanisa na Serikali. Maendeleo ya kisheria yaliyofuata hayajabadilisha utiifu wao wa sheria ya 1905, kama ilivyothibitishwa na Waziri Mkuu Elisabeth Borne mnamo Machi 2023.

Kardinali Parolin anasindikizwa kwenye mkutano huo Alhamisi tarehe 16 Januari 2025, na Balozi wa Vatican Celestino Migliore, pia  alikuwepo rais wa Baraza la Maaskofu wa Ufaransa, Askofu Mkuu Éric de Moulins-Beaufort, Askofu Mkuu wa Reims. Alhamisi saa  12.30 jioni, kutakuwa na mkutano kati ya Waziri wa Mambo ya Nje na Waziri Mkuu wa Ufaransa, François Bayrou, ambao utafanyika katika Hoteli ya Matignon. Tovuti ya Serikali ilibainisha kuwa pamoja na Mkutano wa kitaasisi, kisha Kardinali  atakwenda katika makao makuu ya Wizara ya Mambo ya Ndani, ambayo mkuu wake, Bruno Retailleau, ataadhimsha pia mia na hatimaye, mkutano umepangwa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Waziri Jean-Noël Barrot kuhusu masuala ya kimataifa yenye maslahi ya pamoja.

16 Januari 2025, 12:00