杏MAP导航

Tafuta

Nembo ya Umoja wa Mataifa (UN) katika Makao yake huko NEW YORK MAREKANI. Nembo ya Umoja wa Mataifa (UN) katika Makao yake huko NEW YORK MAREKANI.  (?Lewis Tse Pui Lung - stock.adobe.com)

Kard.Parolin mjini New York kwa Mkutano Mkuu wa 79 wa Umoja wa Mataifa

Kwa mujibu wa taarifa kutoka @TerzaLoggia,Katibu wa Vatican,Kardinali Parolin,atakuwa Marekani kuanzia tarehe 22 hadi 30 Septemba 2024 na atashiriki katika matukio ya Juma la Ngazi ya Juu 2024.Misa imepangwa kufanyika kwa ajili ya miaka 60 ya Makao Makuu ya Ubalozi wa Vatican katika Umoja wa Mataifa.

Vatican News

Kuanzia Dominika tarehe 22 Septemba hadi Jumatatu tarehe 30 Septemba 2024, Katibu wa Vatican, Kardinali Pietro Parolin, atakwenda New York kushiriki Kikao cha 79 cha Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa. Hii ilijulikana kutoka katika chapisho la Umoja wa Mataifa huko New York, Marekani. Kardinali Parolin pia ataadhimisha Misa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 60 ya Ubalozi wa Vatican katika Umoja wa Mataifa.

Mkutano Mkuu wa 79 wa Umoja wa Mataifa utajikita katika kukuza masuluhisho ya pande nyingi kwa kuzingatia Mkataba wa Umoja wa Mataifa na kuongeza kasi ya juhudi za kutekeleza Ajenda ya 2030 ya Malengo ya Maendeleo Endelevu. Miongoni mwa vipaumbele ni uungaji mkono wa amani na usalama wa kimataifa, kukuza maendeleo endelevu, mapambano dhidi ya mabadiliko ya tabianchi, upotevu wa viumbe hai na uchafuzi wa mazingira.

Kard.Parolin huko UN , New York Marekani
21 Septemba 2024, 10:58