杏MAP导航

Tafuta

Baadhi ya mapadre  na vijana tayari wako Lisbon. Baadhi ya mapadre na vijana tayari wako Lisbon. 

GCE itakuwa Lisbon kwa WYD inayohamasishwa na Baraza la Kipapa la Elimu na Utamaduni

Siku ya 37 ya Vijana Duniani itafanyika kuanzia tarehe 1 hadi 6 Agosti 2023 huko Lisbon,Ureno.Katika muktadha huo,pamoja na Papa Francisko na vijana kutoka ulimwenguni kote,watazindua kwa upya Mkataba wa Kimataifa wa ahadi za Elimu(GCE)kama ulivyaonzishwa na Papa 2019.

Na Angella Rwezaula, - Vatican.

Katika siku ya XXXVII Vijana Duniani  2023 inayoanza tarehe 1 hadi 6 Agosti 2023 huko Lisbon nchini Ureno. Baraza la Kipapa la Elimu na Utamaduni, linatoa taarifa kuwa litakuwapo katika Siku ya Vijana Duniani (WYD)ambapo limeamua kutumia fursa hiyo kwa kuzindua kwa upya  yale ambayo Baba Mtakatifu Francisko  aliyaanzisha mnamo  mwaka 2019 ili kujenga Mkataba wa Kimataifa wa Elimu kwa manufaa ya vizazi vijana na kupitia kwao, iwe  dunia nzima. Kwa maana hiyo, shughuli zifuatazo zimepangwa kama sehemu ya Siku ya vijana (WYD): Watakuwepo katika Jiji la Furaha na Stendi inayolenga kuonesha Mkataba wa Kimataifa, kwa lengo  kufanya Mkataba wa Kimataifa  wa Elimu ujulikane  lakini zaidi ya yote katika kuvutia vijana wageni  (kupitia shughuli zenye  msimamo na pia uchunguzi wa mtandaoni) maoni, mawazo na mapendekezo juu ya elimu na matarajio ya siku zijazo.

Vijana wageni watawaalika kushiriki uzoefu wa ziara yao kwenye stendi kwa kutumia:#globalcompactoneducation katika historia zao, Post na Reel, kwa kutumia:@globalcompactoneducation, Instagram au @GConEducation katika Twitter. "Tutaomba hata utengeneze Reel/video (angalau ya sekunde 90) kuhusu uzoefu muhimu wa kielimu ambao umeshiriki na kututumia kwa kupitia: info@educationglobalcompact.org: na uzoefu wa kuvutia zaidi utahamasishwa  kwenye tovuti: . Tarehe 1 Agosti kuanzia saa 2.30 asubuhi hadi saa 10 jioni katika Ukumbi wa Chuo Kikuu cha Kikatoliki cha Ureno kama sehemu ya mipango ya “Nyumba ya Uchumi wa Francisko” kutakuwa na mkutano wa (Global Compact) wa  Mkataba wa  kielimu Kimataifa ambapo utaingiliwa kati kama mzungumzaji mkuu. Mnamo tarehe 2 Agosti kuanzia saa 3 asubuhi hadi saa 10 jioni katika Ukumbi wa Kitivo cha Chuo Kikuu cha Lisbon, kama sehemu ya mipango ya Tamasha la Vijana, mkutano utafanyika juu ya mada: “Tumaini. Wito wa kuelimisha” unaohamasishwa na Baraza la Kipapa la Elimu na Utamaduni  pamoja na kikundi cha maprofesa kutoka shule za Kikatoliki za Ureno ambapo, kupitia ushuhuda fulani, watazingatia jukumu la msingi kuelimisha na jinsi ilivyo muhimu kwa vijana wenye vipaji kuzingatia aina hizi za kazi.

Tarehe 3 Agosti 2023 saa tatu kamili  asubuhi katika mchakato wa mkutano aliofanya Baba Mtakatifu pamoja na wanafunzi wa chuo kikuu cha Kikatoliki cha Ureno kutakuwa na ushuhuda wa mwanafunzi kijana kuhusu uzoefu wa Global Compact na wanajua kwamba Baba Mtakatifu atagusa mpango huu katika hotuba yake tarehe 4 Agosti saa 2.30 usiku katika Jiji la Furaha kutakuwa na ushuhuda juu ya Mkataba wa Elimu Kimataifa. Kwa maelezo zaidi bonyeza:  

Mkataba wa kielimu kimataifa utakuwa na nafasi katika WYD
31 Julai 2023, 11:09