杏MAP导航

Tafuta

Hija ya kitume Papa Francisko nchini Iraq:Mwenyeheri siyo shujaa ni shuhuda

Vijana wa Jumuiya ya Kikaldayo,wamejiandaa kikamilifu kwa muda mrefu kwa nyimbo zao wakisubiri kumpokea.Papa Francisko na wote waliomzunguka wanaonesha jinsi walivyo na mavazi rasmi meupe yaliyoandaliwa kwa fursa hii.Video fupi inaonesha ufupisho huo wa misa takatifu.Pia pia video nyingine fupi inaonesha wakati wanasubiri Papa katika Kanisa kuu.

Na Sr. Angela Rwezaula-Vatican.

Yesu anabadilisha historia na nguvu ya unyenyekevu ya upendo.Mwenye mara nyingi siyo shujaa bali ni shuhuda daima. Ni kutoka katika takari ya mahubiri ya Papa Francisko wakati wa Misa takatifu iliyofanyika katika Kanisa kuu la jijini Baghdad kwa kuhitimish siku yake ya pili ya ziara yake ya kitume, Papa mejikita kwenye tafakari juu ya maana ya 'Heri za mlimani' na amewahimiza waamini kushuhudia kila siku ule mtindo wa maisha unaoongozwa na Yesu na ambao unapindua mawazo ya wanadamu. Katika Video Fupi inaoenesha ufupisho wa misa hiyo takatifu katika Kanisa Kuu la  Baghdad na yenye maana kuu katika ziara hiyo ya Kitume nchini Iraq, iliyoanza Ijumaa, tarehe 5 na itahitimishwa tarehe 8 Machi 2021.

WAAMINI WAKIWA WANAMSUBIRI PAPA KATIKA MAADHIMISHO YA MISA TAKATIFU

Sehemu ya pili ya Video inaonesha wakati waamini wako tayari wanamsubiri Papa Francisko kuadhimisha Misa katika Kanisa Kuu, jijini Baghdad akiwa katika ziara hii ya kitume kwa siku tatu. Lugha zilizoambatana na sherehe ya Ekaristi hiyo zilikuwa ni Kiitaliano, Kikaldayo na Kiarabu na katika maombi ya waamini pia  ilikuwa ni lugha ya kiharamu, Kurdish, Turkmen na Kiingereza. Kuna maneno matatu muhimu yaliyomo kwenye mahubiri ambayo Papa Francisko amefafanua kwa Kiitaliano na ambayo yamependekezwa na Masomo yaliyosomwa yaani:hekima, shahidi na ahadi.

 

06 Machi 2021, 18:11