杏MAP导航

Tafuta

2025.08.27 Mama wa Neema huko Velletri 2025.08.27 Mama wa Neema huko Velletri  (credits sito web diocesi Velletri-Segni - Frascati)

Velletri kutangazwa Jiji la Maria.Papa:Na iwe ni chachu ya ushuhuda wa Injili

Katika ujumbe wake uliotiwa saini na Kardinali Pietro Parolin Katibu Mkuu wa Vatican,Papa Leo XIV anahimiza kuishi maisha ya kukaribisha,hasa wale walio katika mazingira magumu zaidi na kutoa mawazo ya pekee kwa wazee na wagonjwa.

Vatican News

Velletri, mji wa eneo la Castelli Romani, umekuwa chini ya vazi la ulinzi na uzazi la Bikira Mtakatifu tangu tarehe 26 Agosti. Na ndiyo tunayosoma katika ujumbe uliotiwa saini na Kardinali Pietro Parolin, Katibu wa Mkuu wa Vatican  ambaye alituma kwa niaba ya Baba Mtakatifu Leo XIV  kwa Askofu wa Velletri-Segni-Frascati, Stefano Russo, katika fursa hiyo ya  Kutatangwa kwa Velletri  kuwa  “Civitas Mariae" yaa “Mji wa Maria”

Katika baraka hiyo inabainisha kuwa: “Baba Mtakatifu Leo XIV anatoa  Salamu za dhati kwa wale ambao watashiriki Maadhimisho makuu, wakati Velletri ikitangazwa  kwa umma kuwa CIVITAS MARIA(“Mji wa Maria.”)Ni matumaini ya  Baba Mtakatifu kuwa tuikio hilo  ambalo Jumuiya inawekwa chini ya vazi  la ulinzi na Umama wa Bikira Maria, liwawezeshe kupyaisha na udhati wa ibada kwa Mama, kwa kuhuisha waamini kuwa mashuhuda wakarimu wa kiinjili, kwa shauku na jitihada ya kuhamasisha wema wa pamoja na kwa kuishi vizuri katika hali ya makaribisho hasa kuelekea watu  wadhaifu zaidi.”

Kwa matashi hayo Baba Mtakatifu anaomba kwa maombezi ya Mama wa Mwokozi , anayeheshimiwa na mji huo kama Mama wa Neema, awape msaada mwingi wa Mbinguni na kwa utashi wake anawatumia Baraka ya Kitume kwa mwashamu, mapadre, Mamlaka ya raia na wote walioko , lakini kwa  wazo maalum kwa wagonjwa na wazee.” Baraka hiyo iliyosaniwa na Kardinali Parolin, Katibu Mkuu wa Vatican, ilitiwa saini tarehe 26 Agosti 2025.

Jana jioni, tarehe 26 Agosti  saa 12.00 jioni masaa ya Ulaya , tangazo la umma na uhamisho wa sanamu ya Mari kwenye Jumba la Jiji, ambapo maandishi ya kumbukumbu yalitolewa, yalifanyika. Hii ilifuatiwa na maandamano hadi Kanisa kuu, ikifuatiwa na Misa  Takatifu iliyoadhimishwa na Askofu Russo. Kwa upade wake  tangazo la "Civitas Mariae" ni "wito kwa ahadi ya pamoja ambayo inaalika kila mmoja wetu kuwa mpatanishi katika maisha yetu ya kila siku na kuishi uwajibikaji pamoja kama ishara thabiti ya imani."

Utambuzi huu unakusudiwa kuwa "dira kwa maisha ya kila mtu," aliongeza Askofu  Russo, "ambayo inaongoza sasa na kufungua njia ya siku zijazo." Wito wa "kuwa jiji la kukaribisha na kushirikisha watu wote," "mwaliko wa kubadilisha tofauti kuwa utajiri na kukuza kukutana kama njia ya matumaini," na kuwa wapenda amani.”

27 Agosti 2025, 18:04