杏MAP导航

Tafuta

Papa Leo XIV ametoa mwaliko kwa wakirsto kusindikiza wagonjwa na kila hali yenye mateso. Papa Leo XIV ametoa mwaliko kwa wakirsto kusindikiza wagonjwa na kila hali yenye mateso. 

Ujumbe wa Papa Leo XIV kwa Siku ya Maisha:Fumbo la mateso linabadilishwa na uwepo wa Bwana!

Katika telegramu iliyotiwa saini na Kardinali Parolin,Katibu Mkuu wa Vatican katika fursa ya Siku ya Maisha inayoadhimishwa na Kanisa la Uingereza na Wales,Scotland na Ireland,Papa Leo XIV aliwataka Wakatoliki kuendelea kutoa ushuhuda wa heshima waliyopewa na Mungu kwa kila mtu bila ubaguzi.

Na Angella Rwezaula – Vatican.

Baba Mtakatifu  Leo XIV alielezea ukaribu wake wa kiroho kwa wale wote wanaoshiriki katika “Siku ya Maisha ya 2025”, iliyohamasishwa na Mabaraza ya Maaskofu Katoliki wa Uingereza na Wales, Scotland na Ireland. Ni katika ujumbe uliotiwa saini na Katibu Mkuu wa Vatican, Kardinali Pietro Parolin. Maadhimisho hayo ya kila mwaka yamejitolea kukuza ufahamu kuhusu maana na thamani ya maisha ya binadamu katika kila hatua na katika kila hali.

Tumaini alikatishi tamaa

Kauli mbiu ya toleo hili la  mwaka  huu ni ile ya Jubilei:  “Tumaini halikatishi tamaa: kupata maana ya kuteseka,” iliyotolewa katika kifungi  cha Warumi 5:5-6, ambapo Mtakatifu Paulo “anatualika kuona kwamba tumaini la Kikristo si tu matumaini yasiyo na maana, badala yake, tumaini lisilotikisika katika uwezo na uwepo wa Mungu aliye pamoja nasi daima.” Katika telegramu yake  iliyoelekezwa kwa Askofu Mkuu John Sherrington wa Liverpool, na mhusika mkuu wa Baraza ka Maaskofu wa Kiingereza na Wales katika masuala ya maisha, Papa Leo XIV anabainisha  kuwa,  kaulimbiu ya Mwaka wa Jubilei, inataka kuvuta hisia za watu jinsi fumbo la mateso, ambalo limeenea sana katika hali ya mwanadamu linaweza kubadilishwa kwa neema kuwa uzoefu wa uwepo wa Bwana.

Kuheshimu maisha
Kuheshimu maisha   (@Vatican Media)

Kwa njia hiyo katika ujumbe wake Baba Mtakatifu  Leo XIV anaendelea kusali kwamba kwa njia ya “ushahidi wa pamoja kuhusu hadhi iliyotolewa na Mungu kwa kila mtu, bila ubaguzi, na kwa kufuatana na Kristo kwa wagonjwa mahututi, wote katika jamii wahimizwe kutetea badala ya kudhoofisha ustaarabu unaosimikwa katika upendo wa kweli na huruma ya kweli.” Papa Leo  XIV anahitimisha ujumbe wake kwa kukabidhi juhudi za wale wanaoshiriki katika siku ya "maombezi ya Mama Yetu wa Shauri Jema" huku akiwapatia Baraka yake ya Kitume kama dhamana ya ujasiri, furaha na amani katika Bwana Mfufuka."

Siku ya maisha
Siku ya maisha

Kwa upande wa Maaskofu wanabinisha kuwa “Tumaini hili, wao wasema, laweza kustahimili giza la kuteseka kwa wanadamu na hata kuona zaidi ya hayo. Maadhimisho ya Siku ya Maisha mwaka huu, Maaskofu wanasema katika Ujumbe wa Maadhimisho haya, ni mwaliko wa kuwaombea wale wanaoteseka na kubaki nao kama Msamaria Mwema, tukishuhudia thamani yao ya kipekee na isiyoweza kurudiwa.”

Papa Leo na Ujumbe kwa Uingereza
15 Juni 2025, 11:08