杏MAP导航

Tafuta

Papa akutana na Rais Mattarella wa Italia

Katika Mkutano wake wa kwanza rasmi katika Jumba la Kituma kati ya Papa na Rais wa Italia akiongoza na mwanae Laura,watoto wake wengine,wajukuu na Uwakilishi wa Serikali ya Italia,miongoni mwa wengine ni Tajan Makamu Waziri Mkuu na Waziri wa Mambo ya Nchi za nje na ya ushirikiano wa kimataifa wa Italia.Mazungumzo yao ya faragaha yalikuwa karibu saa moja.Papa na Rais wa Italia walikuta katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro mwishoni mwa Misa ya kuanza Upapa wake.

Na Angella Rwezaula – Vatican.

Ijumaa tarehe 6 Juni 2025, Baba Mtakatifu Leo XIV alikutana katika Jumba la Kitume mjini Vatican na Rais wa Jamhuri ya Italia, Bwana Sergio Mattarella, ambapo mara baada ya Mkutano huo alikutana na Kardinali Pietro Parolin, Katibu Mkuu wa Vatican akiambatana na Monsinyo  Miros?aw Wachowski, Katibu Msaidizi wa Vatican wa Mahuhusiano,Ushirikiano na Mataifa na Mashirika ya Kimataifa.

Wakati wa Rais Kusindikizwa katika ofisi ya Papa
Wakati wa Rais Kusindikizwa katika ofisi ya Papa   (@Vatican Media)
Papa Leo akimpokea mgeni wake Rais wa Italia
Papa Leo akimpokea mgeni wake Rais wa Italia   (@Vatican Media)

Kwa mujibu wa taarifa za Vyombovya habari Vatican zimebainisha kuwa: “Wakati wa majadiliano mazuri katika Sekretarieti ya Nchi, kuridhika kulioneshwa kwa mahusiano mazuri baina ya nchi hizo mbili. Mtazamo ulikuwa katika masuala ya kimataifa, na kipaumbele maalum kwa migogoro inayoendelea katika Ukraine na Mashariki ya Kati. Mazungumzo yaliendelea na baadhi ya masuala ya kijamii, kwa kurejeea kwa namna ya pekee  mchango wa Kanisa katika maisha ya nchi.”

Wakati wa mazungumzo
Wakati wa mazungumzo   (@Vatican Media)
Wakati wa kubadilishana zawadi
Wakati wa kubadilishana zawadi   (@Vatican Media)

Walipofika mjini Vatican, muda mfupi kabla ya saa 3.00 asubuhi, kwa gari, akiingia kutokea nia ya Arco delle Campane, baada ya kuvuka Njia ya  Conciliazione, ambayo ilikuwa imefungwa kwa umma tangu asubuhi.

Walioandamana na rais kwenye Jumba la Kitume walikuwa binti yake Laura na watoto wake wengine wawili, pamoja na wenzi wao wa ndoa na wajukuu watano. Na Wajumbe waliofuatana naye, miongoni mwa wengine, ni Waziri wa Mambo ya Nje na Makamu Rais wa Baraza laMawaziri Italia, Bwana Antonio Tajani, Balozi wa Italia katika Mji wa Vatican  Francesco Di Nitto, na Katibu Mkuu wa Ikulu ya Rais Bwana Ugo Zampetti.

Rais wa Italia, mtoto wake na Papa Leo XIV
Rais wa Italia, mtoto wake na Papa Leo XIV   (@Vatican Media)

Wakati wa kusubiriwa kwenye uwanja wa  Mtakatifu  Damas alikuwa Mwakilishi Mkuu wa Mji wa Vatican wa nyumba ya Kipapa, Monsinyo Leonardo Sapienza, pamoja na Kikosi cha kijadi cha  Walinzi wa Uswiss uliotumwa pamoja wahudumu wa Baba Mtakatifu. Mabadilishano ya salamu, kubadilishana Nyimbo za Kitaifa, kisha Rais Mattarella akafikia Loggia ya pili kwa lifti katika mkutano na Papa Leo XIV katika Maktaba ya Jumba la Kitume.

Picha ya Pamoja na kundi zima kikundi kilichomsindikiza Rais wa Italia kwa Papa
Picha ya Pamoja na kundi zima kikundi kilichomsindikiza Rais wa Italia kwa Papa   (@Vatican Media)
06 Juni 2025, 16:29