杏MAP导航

Tafuta

2025.06.05 Papa Leo alikutan na Bwana Kiko Arguello Mwanzilishi wa Harakati ya Neocatekumenali. 2025.06.05 Papa Leo alikutan na Bwana Kiko Arguello Mwanzilishi wa Harakati ya Neocatekumenali.  (@Vatican Media)

Papa Leo XIV akutana na wakuu wa Harakati ya Neokatekumenali

Baba Mtakatifu tarehe 5 Juni 2025 alikutana kwa mara ya kwanza na Bwana Kiko Argüello mjini Vatican,Padre Mario Pezzi na Maria Ascensión Romero waliowasilisha kazi ya uinjilishaji katika mabara matano.

Vatican News

Furaha na shukrani. Hizi ndizo hisia ambazo timu ya kimataifa ya Harakati ya Neokatekumenali, ukweli wa kikanisa ulioenea katika mabara matano, ulioneshwa kwa Baba Mtakatifu  Leo XIV katika Mkutano wa kwanza wa faragha uliofanyika tarehe 5  Juni 2025 katika Jumba la Kitume mjini Vatican.

Papa na Bwana Kiko
Papa na Bwana Kiko   (@Vatican Media)

Baba Mtakatifu Leo  XIV alipewa nakala ya Picha ya Bikira wa Njia, ambayo iko katika Kanisa Kuu la Madrid nchini Hispania, ambapo  ina maneno yaliongoza utume wa safari ya imani yaliyoandikwa: "Lazima tuunde jumuiya kama Familia Takatifu ya Nazareti, wanaoishi kwa unyenyekevu, urahisi na sifa. Mwingine ni Kristo.” Papa pia alipewa nakala  nyingine ya kitabu kilichochapishwa hivi karibuni, chenye kichwa: “Cuore indiviso, missione e verginità”, yaani, " Moyo usiogawanyika, Utume na usafi,” ambacho kina nukuu zaidi ya 400 kuhusu wanawake na mwanzilishi Carmen Hernández.

Wakati wa mkutano wao
Wakati wa mkutano wao   (VATICAN MEDIA Divisione Foto)

Uhusiano na Mama Yetu wa Pompei

Mwanzilishi wa Harakati hiyo, Bwana Kiko Argüello kwa mujibu wa taarifa kutoka katika Harakati hiyo inaarifu kwamba  alisema alivyofurahi sana kwamba Papa alikuwa mmisionari, kuhusiana na chapa yenye nguvu ya kimisionari ya Harakati ya Neokatekumenali. Papa, aliyechaguliwa mnamo tarehe 8 Mei 2025 ambayo ilikuwa ni siku ya Sala  kwa Mama Yetu wa Rozari wa Pompei, aliambiwa juu ya dhamana ya kina ya Harakati ya Neokatekumenali na maadhimisho haya. Bwana Kiko Argüello na Carmen Hernández walipofika Roma mwaka wa 1968, kwa hakika, walikwenda Pompei kumwomba Bikira wa Rozari kulinda na kuunga mkono utume wao. Hasa mnamo tarehe 8 Mei 1974, kwa mara ya kwanza, mwishoni mwa Katekesi ya Papa Paulo VI aliwasalimu mapadre na walei waliohudhuria wa Harakati ya Neokatekumenali, "akituambia maneno ya kinabii ambayo yalikuwa ya msaada mkubwa kwa Harakat hii," Kiko alikumbuka.

Ugeni wa Neokatekumenali
Ugeni wa Neokatekumenali   (@Vatican Media)

Kuanzishwa kwa Kikristo katika majimbo na parokia

Katika mkutano huo, "karibu sana", taarifa kwa vyombo vya habari inaendelea, "Timu iliweza kumsasishia Papa kuhusu shughuli nyingi ambazo Harakati inafanya katika Kanisa, kwa njia ya Ratiba ya Ukristo inayotolewa kwa Parokia na Majimbo, kusaidia familia katika kukabiliana na changamoto ya ulimwengu mamboleo, kuishi wito wao, kufungua maisha katika utimilifu, kutoa fursa kwa vijana wengi kukutana na Yesu Kristo.”

Uinjilishaji duniani

Timu ya Kimataifa ya Harakati hiyo ilipata fursa ya kumjulisha Papa Leo XIV  kuhusu kazi ya uinjilishaji ambayo wasafiri wengi wanaifanya katika majimbo mengi, kuhusu “idadi kubwa ya familia ambazo, kwa kumshukuru Bwana, zimejitolea kusaidia utume wa Kanisa katika maeneo maskini na magumu zaidi duniani.” Kuhusu “kuwapo kwa Harakati hiyo katika nchi 138” na kuhusu “idadi ya seminari za Redemptoris Mater (Mama wa Mkombozi) zinazofunguliwa sasa katika majimbo zaidi ya mia moja kwenye mabara 5 yenye waseminari wengi wanaojiandaa kuwa mapadre.” Taarifa ilibanisha kuwa Papa  aliwahimiza  “kuendelea na utume huu adhimu kwa maisha ya Kanisa.”

NEOCATEKUMENALI
07 Juni 2025, 14:10