杏MAP导航

Tafuta

2025.06.07 Papa Leo XIV na Bwana Javier Gerardo Milei, Rais wa Jamhuri ya Argentina. 2025.06.07 Papa Leo XIV na Bwana Javier Gerardo Milei, Rais wa Jamhuri ya Argentina.  (@VATICAN MEDIA)

Mkutano wa Papa na Rais Milei wa Argentina

Baba Mtakatifu Leo XIV amekutana na Rais wa Jamhuri ya Argentina ambao mara baada ya Mkutano huo amefanya mazungumzo na Sekretarieti ya Vatican kwa kutazama juu ya mwenendo wa kisiasa na kiuchumi,juu ya mapambano dhini ya umaskini na jitihada kwa ajili ya maisha ya kijamii.Hasa kwa umakini hata wa migogoro inayoendelea huku wakionesha umuhimu wa dhamira.

Vatican News

Jumamosi tarehe 7 Juni 2025, Baba Mtakatifu Leo XIV amekutana katika Jumba la Kitume mjini Vatican na Rais wa Jamhuri ya Argentina, Bwana Javier Gerardo Milei. Kwa mujibu wa taarifa kutoka Vyombo vya Habari  vya Vatican imeripoti kwamba,  mkuu wa nchi ya Argentina mara tu baada ya mkutano huo na Baba Mtakatifu, pia alikutana na Kardinali Pietro Parolin, Katibu Mkuu wa Vatican akiambatana na Monsinyo Miros?aw Wachowski, Katibu Msaidizi wa Mahusiano, Ushirikiano  na Mataifa na Mashirika ya Kimataifa.

Papa na Rais wa Argentina na wasindikizaji wake
Papa na Rais wa Argentina na wasindikizaji wake   (@VATICAN MEDIA)

"Wakati wa majadiliano ya kina katika Sekretarieti ya Vatican, kuthaminiana kwa mahusiano thabiti ya nchi mbili na nia ya kuyaimarisha zaidi kulithibitishwa,” kwa mujibu wa Ofisi ya Habari ya Vatican. Kisha majadiliano yalilenga katika “masuala ya maslahi ya pamoja, ikiwa ni pamoja na mwelekeo wa kijamii na kiuchumi, mapambano dhidi ya umaskini na kujitolea kwa mafungamano ya kijamii.”.

Papa Leo wakati wa kubadilishana zawadi
Papa Leo wakati wa kubadilishana zawadi   (@VATICAN MEDIA)

Na tena, “baadhi ya masuala ya kijamii na kisiasa ya kikanda na kimataifa yalishughulikiwa ikiwa ni pamoja na  umakini maalum kwa migogoro inayoendelea, wakionesha umuhimu wa dhamira ya haraka ya kuunga mkono amani."

Rais Milei na Kardinali Parolin
Rais Milei na Kardinali Parolin   (@VATICAN MEDIA)
Rais Milei na Sekretarieti ya Vatican.
Rais Milei na Sekretarieti ya Vatican.   (@VATICAN MEDIA)
07 Juni 2025, 14:11