杏MAP导航

Tafuta

2022.05.23 Madhabahu ya Sheshan nchini China 2022.05.23 Madhabahu ya Sheshan nchini China 

Papa Leo XIV:kwa maombezi ya Maria tuombee watu wote wanaoteseka!

Mara baada ya sala ya Malkia wa Mbingu Papa Leo XIV amekumbuka kutangazwa kuwa wenyeheri Padre Stanislaus Kostka Streich aliyeuwawa 1938;Siku kuu ya kiliturujia ya Bikira Maria Msaada wa Wakristo,sambamba na Siku ya Kuombea Kanisa nchini China.Kwa hisia hizi maombi yetu yanawakumbatia watu wote wanaoteseka kwa sababu ya vita.Papa amekumbuka miaka 10 ya Waraka wa Papa Francisko wa Laudato si kuhusu utunzaji wa nyumba yetu ya pamoja.

Na Angella Rwezaula – Vatican.

Baba Mtakatifu Leo  XIV,  mara baada ya sala ya Malkia wa Mbingu akiwageukia waamini na mahujai wengi waliofika katika Uwanja wa Mtakatifu Petro mjini Vatican, Dominika tarehe 25 Mei 2025 alisema “ Wapendwa kaka na Dada! Jana huko Poznań (Poland) Stanislaus Kostka Streich alitangazwa kuwa mwenyeheri, Padre wa jimbo aliyeuawa kwa kuchukiwa imani mwaka 1938, kwa sababu kazi yake kwa niaba ya maskini na wafanyakazi iliwakasirisha wafuasi wa itikadi ya kikomunisti. Mfano wake uweze kuwatia moyo hasa mapadre kutumikia kwa ukarimu kwa ajili ya Injili na kwa ajili ya ndugu zao.”

Padre aliyetangazwa Mwenyeheri huko Poland
Padre aliyetangazwa Mwenyeheri huko Poland

Papa akiendelea alisema “Pia jana(Jummosi 24 Mei 2025), iliadhimishwa  kumbukumbu ya kiliturujia ya Bikira Maria Msaada wa Wakristo, sambamba na Siku ya Kuombea Kanisa nchini China, iliyoanzishwa na Baba Mtakatifu Benedikto wa kumi na sita. Katika makanisa na vihekalu vya China na duniani kote, sala ziliinuliwa kwa Mungu kama ishara ya kujali na upendo kwa Wakatoliki wa China na ushirika wao na Kanisa la ulimwengu wote. Kwa njia hiyo Maombezi ya Maria Mtakatifu zaidi yapate kwa ajili yao na kwetu sisi neema ya kuwa mashuhuda wa Injili wenye nguvu na furaha, hata katikati ya majaribu, ili kudumisha amani na maelewano daima,” Papa Leo alisisitiza.

Maria wa Sheshan nchini China
Maria wa Sheshan nchini China

Kwa kuongeza alisema “Kwa hisia hizi maombi yetu yanawakumbatia watu wote wanaoteseka kwa sababu ya vita; tunaomba ujasiri na ustahimilivu kwa wale wanaojishughulisha na mazungumzo na kutafuta amani kwa dhati.” “Miaka 10 iliyopita Papa Francisko alitia saini Waraka wa Laudato, unaojikita juu ya utunzaji wa nyumba yetu ya pamoja. Imekuwa na mtawanyiko wa ajabu, ikihamasisha juhudi nyingi na kufundisha kila mtu kusikiliza kilio cha pande mbili za Dunia na maskini. Ninawasalimia na kuwatia moyo Harakati ya Laudato si’ na wale wote wanaotekeleza ahadi hii.

Baba Mtakatifu Leo XIV kadhalika alitoa salamu: “Ninawasalimu ninyi nyote kutoka Italia na kutoka sehemu nyingi za dunia, hasa mahujaji kutoka Valencia na wale kutoka Poland, kwa baraka kwa wale wa Poland ambao wanashiriki katika hija kuu ya Madhabahu ya Maria wa Piekary ?l?skie.

Mahujaji katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro
Mahujaji katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro   (@Vatican Media)

Nawasalimu waamini wa Pescara, Sortino, Paternò, Caltagirone, Kaskazini Massarosa, Malnate, Palagonia na Cerello, na wale wa parokia ya Mioyo Mitakatifu ya Yesu na Maria huko Roma. Ninawasalimu kwa upendo vijana wa Jimbo Kuu la Genova, vijana wa kimapimara wa Mtakatifu Teodori, katika Jimbo la Tempio-Ampurias, waendesha baiskeli wa Paderno Dugnano na Bersaglieri wa Palermo.” Kwa kuhitimisha aliwatakia Dominika njema!

Baada ya sala ya Malkia
25 Mei 2025, 16:05