杏MAP导航

Tafuta

2025.05.19 Papa alikutana na Bwana Anthony AlbaneseWaziri Mkuu wa Australia 2025.05.19 Papa alikutana na Bwana Anthony AlbaneseWaziri Mkuu wa Australia   (@VATICAN MEDIA)

Papa akutana na Waziri Mkuu wa Australia

Alasiri Mei 19,Papa Leo XIV amekutana na Waziri Mkuu wa Jumuiya ya Madola ya nchi kubwa ya Oceania Anthony Albanese.Katikati ya mazungumzo na Askofu Mkuu Gallagher,Katibu wa Mahusiano na Mataifa na Mashirika ya Kimataifa pia ni kuhusu ulinzi wa mazingira,maendeleo fungamani ya binadamu,uhuru wa kidini na mchango wa Kanisa Katoliki katika huduma kwa jamii.

Vatican News.

Jumatatu 19 Mei 2025 Baba Mtakatifu Leo XIV alikutana katika Jumba la Kitume mjini Vatican, na Waziri Mkuu wa Jumuiya ya Madola ya Australia, Mheshimiwa Anthony Albanese, ambaye baadaye alikutana na  Askofu Mkuu Paul Richard Gallagher, Katibu wa Mahusiano na Mataifa na Mashirika ya Kimataifa.

Papa na Waziri Mkuu wa  Australia Papa Leo XIV
Papa na Waziri Mkuu wa Australia Papa Leo XIV   (@VATICAN MEDIA)

Wakati wa mazungumzo ya  dhati yaliyofanyika katika Sekretarieti ya Vatican, shukrani za dhati zilioneshwa kwa uhusiano mzuri wa nchi mbili kati ya Vatican na Australia, pamoja na mchango wa Kanisa Katoliki katika huduma kwa jamii, hasa katika nyanja ya elimu.

Waziri Mkuu wa Australia na Katibu wa Vatican wa mahusiano na nchi na mashirika ya kimataifa
Waziri Mkuu wa Australia na Katibu wa Vatican wa mahusiano na nchi na mashirika ya kimataifa   (@VATICAN MEDIA)

Kisha mabadilishano ya maoni yalifanyika kuhusu hali ya kijamii na kisiasa ya nchi, yakilenga hasa mada zenye maslahi kwa pande zote mbili, zikiwemo ulinzi wa mazingira, maendeleo fungamani ya binadamu na uhuru wa dini.

Papa na waziri Mkuu wa Australia
19 Mei 2025, 21:36