杏MAP导航

Tafuta

Papa Francisko aliandaa ujumbe wa Video katikati ya 2024 kwa ajili ya tamasha la maisha (Viate fest)nchini Mexico kwa mwaka huu. Papa Francisko aliandaa ujumbe wa Video katikati ya 2024 kwa ajili ya tamasha la maisha (Viate fest)nchini Mexico kwa mwaka huu. 

Mexico:mamiaelfu ya vijana wasikiliza kwa mara nyingine sauti ya Francisko

Wakati wa maadhimisho makubwa ya tamasha la Maisha nchini Mexico,walionesha video ya Papa aliyokuwa amerekodi katikati ya 2024.Katika muktadha wa Jubilei ya matumaini,Papa kwa mara nyingine tena aliwaalika vijana kupaza sauti kubwa na kujitahidi katika mabadiliko ya ulimwengu.

Vatican News

Zaidi ya vijana 100,000 wameunganika katika Zócalo ya mji wa Mexico, uwanja mkuubwa sana wa taifa la Amerika Kusini kwa ajili ya kusheherekea tamasha la maisha (Viate fes) na hasa kwa ajili ya jitihada za kuhamasisha amani na maridhiano katika watu ulimwenguni. Katika fursa ya onesho la kisanii ndani yake ambao kwa namna ya pekee limewapa hisia  kali ni lile wa kuwawekea ujumbe wa video ambao Papa Francisko aliyefariki siku kumi nanne zilizopita(21 Apeili) alikuwa amerekodi kwa ajili ya tukio hilo mouhimu  katikati ya mwaka 2024.

Ujumbe wa Papa Francisko kwa vijana wa Mexico uliorekodiwa katikati ya 2024

“Ninajua kwamba mmeunganika katika Zócalo. Na mmeunganika ili kupokea na kutoa. Hamko pale kukaa kimya, bali kwa ajili ya kupaza sauti, kusongesha  vitu mbele, kwa furaha, kwa ajili ya kupokea ujumbe na kuueneza ujumbe huo. Ninawashukuru kwa utashi wenu huu wa kutenda. Kwa sababu, kuna mambo mengi mabaya, katika ulimwengu na tunapaswa kuutuliza. Lakini pia kuna mambo mazuri na  ni ninyi ambao mko hapo mmeunganika, kwa sababu mnatamani kitu zaidi.” Ndiyo maneno ya Papa Francisko

Tumaini kwa ajili ya Ulimwengu

Katika mwaka ambao Kanisa Katoliki linaadhimisha Jubilei ya Matumaini(2025), wale wote waliokusanyika katika tamasha hili walikuwa wamevaa leso vyeupe, ishara ya kuchangamka kwa vijana na shauku ya pamoja ya kurudisha uwezo wa kuzungumza kwa ajili ya kijenga jamii ya ududu zaidi na mshikamano. Kwa njia hiyo Papa Francisko alikuwa amesema:

"Msisahau kamwe leso nyeupe ambayo mnaona, ambayo inazungumza juu yenu: leso nyeupe ni  tumaini daima lawadhambi wote, kama sisi. Na Mungu awabariki na Bikira wa Guadalupe  awalinde na msisahau kusali kwa ajili yangu. Asante,” alihitimisha ujumbe wake.

Ujumbe wa Papa kwa vijana wa Mexico uliokuwa umeandaliwa tangu katikati ya 2024
04 Mei 2025, 12:00