杏MAP导航

Tafuta

Siku kuu ya Rita,huko Cascia na salamu za Papa Leone XIV. Siku kuu ya Rita,huko Cascia na salamu za Papa Leone XIV. 

Cascia:Siku kuu ya Mtakatifu Rita kwa baraka na salamu za Papa Leo XIV

Mamma ya watu walikusanyika tarehe 22 Mei katika Madhabahu ya Kipapa ya mji wa Umbrian katika kumbukizi ya kiliturujia ya Mtakatifu Rita wa Cascia.Mkuu wa Shirika la Mtakatifu Agostino aliwapa waamini ujumbe kutoka kwa Papa Leo XIV:"Aliniomba niwape salamu zake na sala yake.Maadhimisho yaliongozwa na Kardinali Reina:'Leo,tukiwa na wasiwasi juu ya kile kinachotokea ulimwenguni kote kuhusu vita vingi visivyoisha,tuombe zawadi ya amani na udugu.'

Na Tiziana Campisi na Angella Rwezaula Vatican.

Salamu na sala kwa waamini na mahujaji ambao tarehe 22 Mei 2025 huko Cascia walifanya kumbukumbu ya kiliturujia ya Mtakatifu Rita. Baba Mtakatifu Leo XIV alimkabidhi Mkuu wa Shirika la Mtakatifu Agostino, Padre Alejandro Moral, aliyeshiriki  misa hiyo, katika Madhabahi ya Kipapa ya mji wa Umbria iliyoongozwa na Kardinali Bardo Reina, Makamu wa Papa, Jimbo la Roma. Mwishoni mwa liturujia, Padre huyo aliwaeleza wale waliokuwapo maneno ya Papa Leo XIV kwamba: “walikutana naye Jumatatu ya Juma hili (Mei 19)akamuuliza kama alikuwa anakwenda Cascia na hivyo akajibu ndiyo na kumtuma salamu yake na maombi yake.

Kardinali Reina aliongoza misa huko Cascia Mei 22
Kardinali Reina aliongoza misa huko Cascia Mei 22

Maelfu ya waridi na sala

Mamia elfu ya watu walikuwepo kwenye Misa hiyo, wakiwa wameshika mawaridi mikononi mwao, maua ambayo ni ishara ya Mtakatifu Rita, yaliyounganishwa na muujiza wa maua ya ajabu, katikati ya kipindi cha baridi sana na theruji, mahali alipozaliwa  Roccaporena, kilomita tano hivi kutoka Cascia; na pia kukumbusha miiba yake na shida alizopata, pamoja na manukato yake. Na ilikuwa hasa kwa misukosuko ya Rita kwamba Kardinali Reina wakati wa mahubiri yake alirejea historia ya maisha yake huku, akikumbuka shida za maisha yake kuanzia: ndoa yake ngumu, mume wake aliyeuawa, watoto wake wawili waliokufa na kisha maisha ya kitawa ambayo mwanzoni hakukubaliwa na  hatimaye kukumbatiwa, lakini kwa mateso mengi na mateso ambayo yalifuatana naye, na mwiba wa maisha yake, hadi mwisho wa maisha yake." Kardinali Reina alisema “angeweza kutumia maovu mengine na pengine pia angepata kibali cha wengine lakini alipendelea njia tofauti, hasa ile  njia ya Injili, ya kupendelea kusamehe.”

Madhimisho ya Mtakatifu Rita wa Cascia
Madhimisho ya Mtakatifu Rita wa Cascia

Zawadi ya Amani

“Tukitazama leo hii, wakati uliowekwa na hali ya  kutisha ya vurugu, ghasia zilizoenea na matukio ya vita ambayo yanatutia wasiwasi kweli, na vita vya tatu vya dunia vilivyomegeka vipande vipande, kama Papa Francisko alivyopendelea kusema”,  Kardinali alisisitiza maneno ya kwanza ya Baba Mtakatifu Leo XIV, ambaye, wakati wa kujitokeza katikati ya dirisha la Baraka ya kwanza ya URB et ORBI,mara baada ya zawadi yake ya amani, alisema: "Leo tuna wasiwasi sana juu ya kile kinachotokea ulimwenguni kote, kuhusu vita vingi ambavyo kiukweli havikomi, kupungua, kuna ongezeko kubwa la jeuri," na  akasisitiza kwamba "uovu hauwezi kushindwa kwa uovu zaidi" na mwaliko wa Papa wa ulikuwa wa “kuondoa silaha za lugha.” Kwa kususitiza zaidi  Papa Leo XIV alisema:"Tunahitaji kupokonya hisia, ili kunyang'anya silaha mioyoni mwetu. Tunahitaji kufikiria njia nyingine za kujenga mahusiano ambayo ni ya kibinadamu kabla ya kuwa ya Kikristo."

Kikanisa cha Roccaporena alikozaliwa Rita kilichoko mlimani alikokuwa akienda kusali njia ya msalaba
Kikanisa cha Roccaporena alikozaliwa Rita kilichoko mlimani alikokuwa akienda kusali njia ya msalaba   (Opera di Santa Rita)

Kutoka kwa Cascia kuna harufu ya udugu ambayo inaweza kung'aa

Kwa upande wa Kardinali Reina akidadavua Injili iliyosomwa ya siku pia alisema “kukaa ndani ya Kristo, katika upendo wake, kama tawi la mzabibu, ndivyo uovu unavyoweza kushindwa, kwa sababu  “Yeyote anayekaa ndani ya Mungu hawezi kutokuwa mwaminifu. Yeyote anayekaa ndani ya Mungu hawezi kudharau wanyonge, yatima, mjane, mgeni, kwa sababu upande wa Mungu daima kuna mema, " alisisitiza, huku akifafanua kwamba "Siri ya Rita ilikuwa hii: alibaki katika Mungu, daima. Mtakatifu Rita alikuwa mwanamke aliyejawa na furaha, hata katika shida. Kwa njia hiyo alihitimisha Kardinali kwa matumaini kwamba kutoka Cascia "harufu ya utakatifu, udugu, wema inaweza kung'aa.”

Roccaporena
Roccaporena   (Opera di Santa Rita)

 

23 Mei 2025, 17:02