杏MAP导航

Tafuta

2025.05.22Askofu Alejandro Labaka Ugarte,mmoja wa watumishi wapya wa Mungu aliyeuawa na Wahindi huko Ecuador mwaka 1987. 2025.05.22Askofu Alejandro Labaka Ugarte,mmoja wa watumishi wapya wa Mungu aliyeuawa na Wahindi huko Ecuador mwaka 1987. 

Kanisa lina watumishi 3 wa Mungu,wamisionari 2 wa Ecuador na Askofu wa Kihindi!

Katika Mkutano wa asubuhi tarehe 22 Mei 2025 kati ya Papa Leo XIV na Kardinali Semeraro,Mwenyekiti wa Baraza la Kipapa la Kuwatangaza watakatifu Papa aliidhinisha Amri kuhusu Askofu Mhispania na mtawa wa Colombia aliyeuawa mwaka 1987 na wenyeji wa Ecuador na mwanzilishi mkuu wa Masista wa kutembelewa kwa Bikira Maria aliyefariki mwaka1914.

Vatican News

Wakati wa mkutano uliofanyika kati ya Kardinali Marcello Semeraro, Mwenyekiti wa Baraza la Kipapa la Kuwatangaza Watakatifu, na Papa Leo XIV, tarehe 22 Mei 2025,  Papa aliidhinisha Baraza hilohilo kutangaza Amri kuhusu watu wafuatao ambao walitoa sadaka ya maisha yao: Awali kwa  Mtumishi wa Mungu Alessandro Labaka Ugarte (Jina: Manuel), wa Shirika la Ndugu Wadogo Wakapuchini,(OFMCap), Askofu wa Pomaria, Mwakilishi wa Kitume wa  Aguarico; alizaliwa tarehe 19 Aprili 1920 huko Beizama (Hispania), na alikufa mnamo tarehe 21 Julai 1987 katika eneo la Tigüino nchini (Ecuador);

Kwa sadaka ya maisha ya Mtumishi wa Mungu, Agnese Arango Velásquez (jina: Maria Nieves de Medellín), wa Shirika la Wakapuchini wa Familia Takatifu; alizaliwa huko Medellín (Colombia) mnamo tarehe 6 Aprili 1937 na kufariki mnamo tarehe 21 Julai 1987 katika eneo la Tigüino (Ecuador);

Kwa mwenye fadhila za kishujaa,  Mtumishi wa Mungu Mathayo Makil, Askofu wa Tralle, Mwakilishi wa  Kwanza wa Kitume wa Kottayam, na Mwanzilishi wa Shirika la Masista wa kutembelewa kwa Bikira Maria; alizaliwa tarehe 27 Machi 1851 huko Manjoor (India) na alikufa tarehe 26 Januari 1914 huko Kottayam nchini (India).

Watumishi wa Mungu wapya
22 Mei 2025, 17:46