杏MAP导航

Tafuta

I misionari Salesiani in India con I giovani. I misionari Salesiani in India con I giovani. 

Papa kwa Wasalesiani:Wasalesiani wana shauku ya Yesu Kristo na kujitolea kwa vijana.Ni mpango mzuri sana!

Katika Ujumbe wa Baba Mtakatifu kwa washiriki wa Mkutano Mkuu wa 29 wa Shrika la Wasalesiani,amemtakiwa kazi njema Mkuu mpya wa shirika Padre Fabio Attard na kushukuru Kardinali Artime kwa huduma iliyotolewa katika miaka hii.Papa amewatia moyo wa kuwa na shauku katikati ya changamoto tofauti kuliko hapo zamani:Imani na shauku hubakia sawa,iliyojaa karama mpya kama vile tamaduni.Shukrani kwa mema mengi yaliyofanywa ulimwenguni kote.

Na Angella Rwezaula – Vatican.

Katika fursa ya Mkutano Mkuu wa XXIX wa Shirika la Wasalesini wa Don Bosco, ulioanza tangu tarehe 16 Februari na utahitimishwa tarehe 12 Aprili 2025, Baba Mtakatifu amewatumia ujumbe wake. Katika Ujumbe huo anaanza kuwaelezea juu ya kutokuweza kukutana nao kwa bahati mbaya,  lakini anawatumia “ujumbe katika fursa hiyo na pia katika maadhimisho ya miaka 150 tangu kutumwa wamisionari wa Kwanza wa Don Bosco nchini Argentina.

Mkutano Mkuu wa 29 wa wasalesiani
Mkutano Mkuu wa 29 wa wasalesiani

Kufuatia na kuchaguliwa kwa Mkuu Mpya wa Shirika, Baba Mtakatifu “anatuma salamu kwa Mkuu mpya wa Shirika hilo, Padre Fabio Attard, akimtakia heri na kazi njema na katika fursa hiyo amemshukuru Kardinali Ángel Fernández Artime aliyeongoza shirika hilo kuanzia(2014-2024), kwa ajili ya huduma ambayo aliwezesha kwa miaka hiyo  na ambapo kwa sasa anaendelea kuitoa katika Kanisa la Ulimwengu," baada ya kuchaguliwa kuwa Kardinali.

Kardinali Artime
Kardinali Artime

Kwa njia hiyo hata akiwa mbali, kwa maana ya kuwa katika nyumba ya Mtakatifu Marta mjini Vatican, Papa Francisko amebainisha kuwa “ningependa kuwahimiza kuishi kwa uaminifu na kujitolea wakati huu wa kusikiliza Roho na utambuzi wa sinodi." Kwa njia hiyo katika mkutano huo wamechagua, kama mada ya kazi yao, yenye kauli mbiu: "Wasalesiani wana shauku kwa Yesu Kristo na kujitolea kwa vijana." Ni mpango mzuri sana: kuwa na "shauku" na "kujitolea", kujiruhusu kushiriki kikamilifu katika upendo wa Bwana na kutumikia wengine bila kujiwekea chochote, kama vile Mwanzilishi wao alivyofanya wakati wake.”

Kituo cha Wasalesiani cha watoto huko Kara
Kituo cha Wasalesiani cha watoto huko Kara

Papa ameongeza kuwa: "Hata kama leo hii, ikilinganishwa na wakati huo, changamoto zinazopaswa kukabili zimebadilika kwa kiasi fulani, imani na shauku inabaki vile vile, iliyojaa karama mpya, kama ile ya tamaduni tofauti." Kwa hiyo Papa anawashukuru "kwa mema wanayofanya duniani kote na anawatia moyo waendelee na uvumilivu." Amewabariki kwa moyo wote na kazi yao ya Mkutano mkuu pamoja na wanashiriki waliotawanyika katika mabara matano na anawaomba tafadhali wamuombee. Mama Maria Msaada wa Wakristo daima awasindikize."

Ujumbe wa Papa kwa Wasalesian
07 Aprili 2025, 11:49