杏MAP导航

Tafuta

2025.04.06 S.E. Jubilei ya wagonjwa na Ulimwengu wa kiafya 2025.04.06 S.E. Jubilei ya wagonjwa na Ulimwengu wa kiafya  (VATICAN MEDIA Divisione Foto)

Papa Francisko:utume wa kiafya siyo rahisi lazima usaidiwe na kuheshimiwa

Katika andiko la Malaika wa Bwana lililotolewa tarehe 6 Aprili 2025,wakati wa Jubilei ya Wagonjwa na Ulimwengu wa Kiafya,matumaini ya Papa ni kupata uzoefu wa mateso ya Mungu yanayojali na kuwaombea madaktari,wauguzi na wahudumu wa afya ambao hawasaidiwi kila mara kufanya kazi katika mazingira muafaka na wakati mwingine ni wahanga wa kushambuliwa.Matumaini yake ni kuwa kuwekeza katika utafiti na katika mfumo jumuishi wa kweli.

Na Angella Rwezaula – Vatican.

Baba Mtakatifu Francisko, Dominika tarehe 6 Aprili 2025, kama kawaida ya kila Dominika ameandaa Mahubiri yake kabla ya sala ya Malaika wa Bwana. Papa anabainisha kuwa Injili ya Dominika ya 5 ya Kwaresima inawakilisha tukio la mwanake aliyefumaniwa katika uzinzi. (Yh 8,1-11). Wakati waandishi na mafarisayo wanataka kumpiga mawe, Yesu anamrudishia mwanamke huyo, uzuri uliopotea. Yeye alianguka katika mavumbi; Yesu katika mavumbi hayo alipitisha kidole chake na aliandika kwa ajili yake historia mpya: ni kidole cha Mungu ambaye anaokoa watoto wake (Es 8,15) na kumukoa katika dhambi( Lk 11,20).

Waamini katika Jubilei ya wagonjwa
Waamini katika Jubilei ya wagonjwa   (VATICAN MEDIA Divisione Foto)

Baba Mtakatifu amebainisha kuwa “kama wakati wa kulazwa, hata sasa katika kuendelea na tiba, ninahisi “kidole cha Mungu” na nafanya uzoefu wake wa bembelezo lake. Katika siku ya Jiblei ya wagonjwa na  ya Ulimwengu wa kiafya, ninaomba Bwana ambaye kwa mguso wa upendo wake uwafikie wale ambao wanateseka na kuwatia moyo wale ambao wanawasaidia. Na ninasali kwa ajili ya madaktari, wauguzi na wahudumu wa kifya, ambao si mara zote wanasaidiwa  katika kazi katika hali inayofaa na wakati mwingine hadi kuwa wahanga wa kushambuliwa. Utume wao siyo rahisi na wanapaswa kusaidiwa na kuheshimiwa. Ni matumaini yangu kuwa wanaweza kuwa rasilimali ya lazima kwa ajili ya tiba na kwa ajili ya utafiti.  Kwa sababu, mifumo ya kifya iweze kuwa jumuishi na makini kwa walio wadhaifu zaidi na walio maskini.”

Misa ya Jubilei ya wagonjwa
Misa ya Jubilei ya wagonjwa   (VATICAN MEDIA Divisione Foto)

Asante wafungwa wa kike Rebibbia

Papa ametoa shukurani kwa matashi mema kutoka kwa wafungwa: “Ninashukuru wafungwa wa magereza ya kike ya Rebibbia kwa kadi ambayo mmenitumia.  Ninasali kwa ajili yao na kwa ajili ya familia zao.”

Siku ya michezo duniani

Katika kumbukizi ya kimataifa Papa amesema “Katika Siku ya Dunia ya Michezo kwa ajili ya Amani na Maendeleo, ninatumaini kwamba michezo itakuwa ishara ya matumaini kwa watu wengi wanaohitaji amani na ushirikishwaji wa kijamii, na ninashukuru vyama vya michezo vinavyoelimisha kikamilifu kuhusu udugu.”

Tuendelee kuombea Ukraine   na Gaza

Kama kawaida ya Papa Francisko hakukosa kutazama vita vilivyosambaa ambapo amesema: “Tuendelee kuombea amani: katika Ukraine inayoteswa, iliyokumbwa na mashambulizi yanayosababisha wahanga wengi wa raia, wakiwemo watoto wengi. Na hali hiyo hiyo inatokea huko Gaza, ambapo watu wanalazimika kuishi katika mazingira yasiyoweza kufikiria, bila makazi, bila chakula, bila maji safi.”

Silaha zinyamaze

Hatimaye ametoa wito wake kuwa “Silaha zinyamaze na mazungumzo yaanze tena; mateka wote lazima waachiliwe na watu lazima wasaidiwe. Tuombe amani katika eneo lote la Mashariki ya Kati; katika Sudan na Sudan Kusini; katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo; huko Myanmar, pia ilikumbwa sana na tetemeko la ardhi; na huko Haiti, ambako vurugu zinaendelea, ambazo ziliua watawa wawili siku chache zilizopita. Bikira Maria atulinde na kutuombea.”

Tafakari la Sala ya Malaika wa Bwana
06 Aprili 2025, 16:02